Posts

Showing posts from October, 2020

SIMBA YAINGIA ANGA ZA UD SONGO, KULIVUTA JEMBE HILI LA KAZI

Image
  IMEFAHAMIKA kuwa, kiungo mshambuliaji wa Simba raia wa Msumbiji, Luis Miquissone, ndiye aliyetoa mapendekezo ya usajili wa kiungo mshambuliaji, Pachoio Lau Há King anayekipiga UD Songo ya nchini huko.   Imeelezwa kuwa, Simba imepanga kumsajili kiungo huyo wa kimataifa raia wa Msumbiji katika kukiboresha kikosi chao kinachojiandaa na Ligi ya Mabingwa Afrika msimu wa 2020/21.   Wakati Simba ikiwa katika mipango hiyo ya kumsajili nyota huyo, imepanga kuachana na kiungo wao mchezeshaji raia wa nchini Kenya, Francis Kahata ambaye mkataba wake unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu.   Kwa mujibu wa taarifa ambazo imezipata Spoti Xtra, Simba inamtumia Luis kufanikisha usajili wa kiungo huyo wa pembeni atakayetua kuichezea timu hiyo kwenye usajili wa dirisha dogo msimu huu.   Mtoa taarifa huyo alisema kuwa, Luis alimpendekeza jamaa huyo baada ya viongozi kumshirikisha kuhusu usajili wa kiungo wa kimataifa mwenye uwezo wa kutengeneza mabao akitokea pembeni. Aliongeza kuwa,

KAZE: HAKUNA MCHEZAJI ANAYEWEZA KUCHEZA MECHI NNE

Image
 CEDRIC Kaze, Kocha Mkuu wa Yanga amesema kuwa hakuna mchezaji wake anayeweza kucheza mechi nne ndani ya siku 12 kutokana na ratiba kuwataka kufanya hivyo jambo ambalo linamlazimu kubadili kikosi mara kwa mara. Kaze ambaye amesaini dili la miaka miwili amekiongoza kikosi cha Yanga kwenye mechi tatu na ameshinda zote ndani ya uwanja na kusepa na jumla ya pointi tisa. Alianza kushinda mbele ya Polisi Tanzania, Uwanja wa Uhuru kwa bao 1-0 kisha alishinda mbele ya KMC kwa mabao 2-1 Uwanja wa CCM Kirumba na jana Oktoba 31 alishinda bao 1-0 dhidi ya Bashara United Uwanja wa Karume, Mara. Kaze amesema:"Nina mechi nyingi na ngumu ambazo ni lazima wachezaji wapambane na wafanye kazi ngumu ya kusaka ushindi lakini hakuna anayeweza kucheza mechi zote nne mfululizo ndani ya kikosi kwa wakati huu wa kusaka ushindi. "Ambacho ninakifanya ni kuona kwamba kila mchezaji anacheza na ninawafanyia mabadiliko wachezaji wangu ili kuona kwamba wanaweza kuwa fiti kwa ajili ya mechi zijazo.

ISHU YA SIMBA KUYUMBA MSIMU WA 2020/21, SIMBA YAFAFANUA

Image
 UONGOZI wa Simba umesema kuwa kwa sasa unaamini kwamba una nguvu ya kutetea taji la Ligi Kuu Bara kwa mara nyingine tena licha ya kuanza kwa kuyumba ndani ya msimu wa 2020/21. Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara amesema kuwa kwenye maisha ya soka kuna mapito ya kipekee ambayo wakati mwingine unashindwa kuwa na chaguo kutokana na matokeo ambayo unayapata jambo ambalo linasababisha timu kuyumba kiasi chake. Kwenye mechi mbili mfululizo zilizopita Simba inayonolewa na Kocha Mkuu, Sven Vandenbroeck ilikuwa kwenye wakati mgumu baada ya kuyeyusha pointi sita jumlajumla ndani ya uwanja. Hali hiyo ilipelekea kufanya mabadiliko kwenye benchi la ufundi kwa kumtimua kocha wa makipa Muharami pamoja na aliyekuwa meneja wa timu hiyo kwa wakati hu Patrick Rweyemamu. Ilifungwa bao 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons na ilinyooshwa ba 1-0 dhidi ya Ruvu Shoting jambo ambalo liliwapa maumivu mashabiki wa Simba pamoja na viongozi kiujumla. Manara amesema:"Kwenye maisha ya soka kuna matokeo magum

RATIBA YA LIGI KUU BARA LEO HII HAPA

Image
 LEO Novemba Mosi Ligi Kuu Tanzania Bara inaendelea kwa mechi mbili ambapo timu nne zitakuwa uwanjani kusaka pointi tatu muhimu namna hii:- Kagera Sugar ambayo imecheza mechi 8 na kujikusanyia pointi 5 itamenyana na Mtibwa Sugar ambayo imecheza mechi 8 na kujikusanyia pointi 11, Uwanja wa Kaitaba. Ruvu Shooting ambayo imecheza mechi 8 na kujikusanyia pointi 12 itakutana na Coastal Union ambayo imecheza mechi  8 na kujikusanyia pointi 9.

CRISTIANO RONALDO APONA CORONA, SASA KAZIKAZI

Image
 UONGOZI wa Juventus umethibitisha kuwa nyota wao Cristiano Ronaldo kwa sasa tayari ameshapona COVID -19 baada ya kubaninika na Virusi hivyo ambapo alikaa karantini kwa muda wa siku 19. Ronaldo akiwa karantini alikosa mechi nne ndani ya kikosi chake ikiwa ni pamoja na ile dhidi ya Barcelona ya mshikaji wake Lionel Messi katika Ligi ya Mabingwa Ulaya wakati wakipoteza kwa kufungwa mabao 2-0. Staa huyo alibainika kupata maambukizi ya Corona akiwa kwenye majukumu ya timu ya Taifa ya Ureno Oktoba 13 mwezi uliopita. "Cristiano Ronaldo amefanyiwa vipimo kwa mara nyingine na amebainika kwamba hana Virusi vya Corona, kwa sasa anarejea kwenye timu hivyo hatajitenga tena kama ilivyokuwa awali." ilieleza taarifa hiyo.

KOCHA MANCHESTER UNITED APATA HOFU KUIKABILI ARSENAL

Image
  OLE Gunnar Solskajer, Kocha Mkuu wa Manchester United amesema kuwa leo Novemba Mosi ana mtihani mzito wa kusaka pointi tatu mbele ya Arsenal. Manchester United ambayo imepoteza mechi mbili Uwanja wa Old Trafford mbele ya Crystal Palace na na Tottenham itawakaribisha tena Arsenal saa 1:30 usiku kusaka pointi tatu muhimu. Arsenal chini ya Kocha Mkuu Mikel Arteta, imeshinda mechi tatu na kupoteza mechi tatu hivyo balaa litakuwa usiku wa leo kwa wababe hawa wawili. Solskajer amesema:"Kwa Arsenal siku zote kupambana nao sio kazi nyepesi ni wagumu na wanahitaji akili zaidi kwa sababu ni timu nzuri ambayo inaongozwa na kocha mzuri." Arteta amesema kuwa anaamini utakuwa ni mchezo mgumu lakini ni lazima vijana wake wacheze kwa nidhamu kupata matokeo chanya.

AZAM FC: TUPO IMARA, TUNA JAMBO LETU

Image
  UONGOZI wa Azam FC umesema kuwa  upo vizuri kwa msimu wa 2020/21 na utafanya mambo tofauti na msimu uliopita ndani ya ligi kuu bara baada ya kumaliza ikiwa nafasi ya tatu na kukosa kutwaa taji lolote lile. Oktoba 30 ikiwa Uwanja wa Azam Complex ilikubali sare ya kufungana bao 1-1 na JKT Tanzania baada ya kutoka kupoteza mchezo wa kwanza mbele ya Mtibwa Sugar kwa kufungwa bao 1-0 Uwanja wa Jamhuri, Moro. Ipo nafasi ya kwanza ikiwa na pointi 22 baada ya kucheza mechi 9 ikitofautiana idadi ya mabao na Yanga ambayo imefunga mabao 11 huku Azam FC ikiwa imefunga mabao 15. Zakaria Thabit, Ofisa Habari wa Azam FC amesema kuwa bado wanajambo lao kwa msimu huu wana amini litatimia kwa kuwa safari ya ligi bado inaendelea. "Bado safari ya ligi inaendelea nasi tuna kazi ya kufanya tunaamini kwamba tutafanya vizuri kwenye kusaka matokeo ndani ya uwanja kwenye mechi zetu zijazo. "Mashabiki watupe sapoti tutafanya vizuri na hatutawaangusha katika hilo kila kitu kinawezekana kw

MSIMAMO WA LIGI KUU TANZANIA BARA UPO HIVI

Image
 MSIMAMO wa Ligi Kuu Tanzania Bara upo namna hii kwa sasa

CHAMA KARUDI NA USHINDI WAKATI SIMBA IKIPIGA MTU 5G UHURU

Image
LABDA unaweza kusema kwamba Simba bila Clatous Chama mambo yanaweza kuwa magumu ila mpira ndio matokeo yalivyo ndani ya uwanja. Baada ya kucheza mechi mbili mfululizo bila kupata matokeo chanya kwa kuyeyusha pointi sita mazima ndani ya uwanja leo Oktoba 31 Simba imeibuka na ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya Mwadui FC. Mechi zake mbili ambazo ni dakika 180 ilichezeshwa ligwaride na Tanzania Prisons, Uwanja wa Nelson Mandela kwa kufungwa bao 1-0 kisha ikanyooshwa tena kwa bao 1-0 dhidi ya Ruvu Shooting Uwanja wa Uhuru na mechi zote mbili Chama hakuwepo kwa kuwa alikuwa anashughulikia paspoti na leo ameanza ndani ya kikosi cha kwanza na Simba ikasepa na pointi tatu.  John Bocco nahodha wa Simba alipachika bao la kwanza dakika ya 25 na la pili alipachika dakika ya 64. Ibrahim Ajibu kiungo mshambuliaji wa Simba amepachika bao lake la kwanza kwa msimu wa 2020/21 ndani ya ligi dakika ya 81 likiwa ni la tatu kwa timu yake leo sawa na  Hassan Dilunga kiungo wa Simba ambaye amepachika bao

BIASHARA UNITED YATULIZWA JUMLAJUMLA NA YANGA, SARPONG AMALIZA MCHEZO

Image
 MICHAEL Sarpong nyota wa kikosi cha Yanga leo ameibuka shujaa baada ya kufunga bao la ushindi mbele ya Biashara United na kuipa pointi tatu muhimu timu yake ambayo haijapoteza mchezo kwa msimu wa 2020/21. Bao hilo la ushindi alipachika dakika ya 68 Uwanja wa Karume, Mara kwa kichwa akimalizia pasi ya nyota wa timu hiyo Ditram Nchimbi na kuituliza kasi ya wapinzani wao Biashara United jumlajumla. Bao hilo linakuwa ni la pili kwa Sarpong ndani ya Ligi Kuu Bara huku likimfanya Nchimbi naye aandike rekodi yake ya kutoa pasi ya kwanza ndani ya ligi kwa msimu wa 2020/21. Ushindi huo unaifanya Yanga kufikisha jumla ya pointi 22 ikiwa nafasi ya pili nyuma ya Azam FC ambayo ikiwa na pointi 22 ila zimetofautiana kwenye idadi ya mabao ya kufunga na kufungana. Azam FC imefunga mabao 15 na Yanga imefunga mabao 11 kwa upande wa mabao ya kufungwa Yanga imefungwa mabao mawili huku Azam FC ikiwa imefungwa mabao manne. Biashara United inashuka nafasi ya nne ikiwa na pointi 16 ikishushwa kut

KOCHA SIMBA ATAJA MATATIZO MAWILI YANAYOKITESA KIKOSI HICHO

Image
JAMHURI Khwelo aliyewahi kuwa kocha wa timu hiyo amesema kuwa kikosi cha Simba kina matatizo makubwa mawili ambayo yanakisumbua kwa sasa jambo ambalo linawafanya wapate matokeo mabovu ndani ya uwanja. Mabingwa hao watetezi wamekutana na vipigo viwili mfululizo na kuziacha alama sita zikisepa na upepo ndani ya Ligi Kuu Bara. Walipoteza mbele ya Tanzania Prisons kwa kufungwa bao 1-0 wakiwa ugenini kwenye Uwanja wa Nelson Mandela kisha wakiwa nyumbani walitembezewa kichapo cha bao 1-0 dhidi ya Ruvu Shooting, Uwanja wa Uhuru. Leo Oktoba 31 Simba ina kibarua cha kusaka pointi tatu muhimu mbele ya Mwadui FC Uwanja wa Uhuru. Julio amesema:"Kwa sasa Simba wanapambana na matokeo magumu kutokana na mambo mawili ambayo wanayo kwanza ni umri wa wachezaji wengi kuwatupa mkono jambo linalowafanya wapate tabu kuhimili mikikimiki ndani ya uwanja. "Pili ni suala la majeruhi wengi ambao wapo kwa Simba kwa sasa, jambo hilo linafanya kocha awe kwenye wakati mgumu kutafuta matokeo na

BIASHARA UNITED V YANGA, NGOMA NI NZITO, CHEKI REKODI ZAO

Image
  IKIWA imepanda Ligi Kuu Bara msimu wa  2018/19 Biashara United leo inakutana na Yanga mara ya tano uwanjani huku rekodi zikiwa ngumu kwa Yanga kupata ushindi Uwanja wa Karume.  Mechi nne ambazo wamecheza, jumla mabao matano yamekusanywa ambapo Yanga imefunga mabao matatu na Biashara United imefunga mabao mawili. Yanga imeshinda mechi mbili na zote ilikuwa nyumbani, Uwanja wa Mkapa huku Biashara United ikishinda mchezo mmoja, wamelazimisha sare moja ilikuwa Uwanja wa Karume. Kwa misimu miwili Yanga haijapata ushindi ndani ya Uwanja wa Karume zaidi ya kuambulia sare ya bila kufungana msimu wa 2019/20 hivyo leo itapambana kuvunja rekodi hiyo. Matoke yao yalikuwa namna hii:-2018/19,Yanga 2-1 Biashara United,  Biashara United 1-0 Yanga . 2019/20 Yanga 1-0 Biashara United. Biashara United 0-0 Yanga.

RATIBA YA LIGI KUU BARA LEO OKTOBA 31

Image
 LEO Oktoba 31 Ligi Kuu Tanzania Bara inaendelea kushika kasi ambapo mechi nne zitachezwa kwa timu nane kusaka pointi tatu ndani ya uwanja. Tanzania Prisons v Polisi Tanzania, Uwanja wa Nelson Mandela, saa 8:00 mchana Namungo FC v Dodoma Jiji, Uwanja wa Majaliwa, saa 10:00 jioni. Biashara United v Yanga, Uwanja wa Karume, saa 10:00 jioni. Simba v Mwadui,saa 10:00 jioni, Uwanja wa Uhuru.

MWADUI FC: TUPO TAYARI KUSAKA POINTI TATU ZA SIMBA

Image
  KHALID Adam, Kocha Mkuu wa Mwadui FC amesema kuwa wapo tayari kwa mchezo wao wa kesho, Oktoba 31 dhidi ya Simba utakaochezwa Uwanja wa Uhuru. Akizungumza na Saleh Jembe, Adam amesema kuwa wanaitambua vema Simba kwa kuwa wamekutana nao mara nyingi uwanjani jambo ambalo linamfanya aamini kwamba watapambana kusaka ushindi. "Tumetoka kupoteza mchezo wetu uliopita imetuumiza ila nimewaambia wachezaji kwamba wasiwe na presha yaliyopita ni muhimu kusahau na kutazama mechi zetu zijazo. "Mchezo wetu dhidi ya Simba ni muhimu kwetu kupata ushindi ili turejeshe hali ya kujiamini na hilo linawezekana ikiwa kila mchezaji atajituma na kusaka matokeo kwa juhudi. "Kikubwa mashabiki wajitokeze kwa wingi kuipa sapoti timu yao na kuona namna ambavyo tutafanya, tupo tayari kwa ushindani," amesema. Timu zote mbili mechi zao za mwisho kwa msimu huu ndani ya Ligi Kuu Bara zimepoteza kwa kuyeyusha pointi tatu. Mwadui FC ilipoteza kwa kufungwa mabao 6-1 dhidi ya JKT Tanzania

KOCHA MPYA SIMBA ANA LESENI YA UEFA, MWENYEWE AFUNGUKA

Image
  TAARIFA zinasema kuwa, Klabu ya Simba, ipo kwenye mazungumzo na Kocha Abdul Idd Salim raia wa Kenya kwa ajili ya kuchukua nafasi ya Muharami Mohammed aliyeondolewa hivi karibuni kikosini hapo.   Muharami ambaye alikuwa akiwanoa makipa wa Simba tangu Julai 2017, amesitishiwa ajira yake kwa kile kilichoelezwa kwamba ameshindwa kuwaongoza vema makipa wa timu hiyo, Aishi Manula, Beno Kakolanya na Ally Salim.   Simba baada ya kuachana na Muharami, wameanza mazungumzo na Salim ambaye kwa sasa anawanoa makipa wa timu ya Sheikh Russel inayoshiriki Ligi Kuu ya Bangladesh.   Salim aliwahi kuwanoa makipa wa Simba katika vipindi viwili tofauti ambapo mara ya kwanza alitua Juni 2015 wakati Kocha Mkuu wa Simba akiwa, Dylan Kerr raia wa England, kisha akaondolewa na kurudi tena Desemba 2016, kipindi Simba ikinolewa na Mcameroon, Joseph Omog ambapo kwenye vipindi vyote alifanya kazi nzuri sana.   Taarifa kutoka ndani ya Simba zinasema kuwa, uamuzi wa kumrudisha kocha huyo ni baada ya

DJOD: JKT TANZANIA WALIWAFUNGA MABAO 6 MWADUI, HAWATATUFUNGA

Image
 RICHARD Djod, nyota wa Klabu ya Azam FC amesema kuwa hawana hofu kwenye mchezo wao wa leo Oktoba 30 dhidi ya JKT Tanzania utakaochezwa Uwanja wa Azam Complex. Azam FC ambao ni vinara wa Ligi Kuu Bara wakiwa na pointi 21 wanamenyana na JKT Tanzania yenye pointi 8 ikiwa nafasi ya 15 zote zimecheza mechi nane. Mchezo uliopita kwa Azam FC ilifungwa kwa bao 1-0 dhidi ya Mtibwa Sugar inakutana na JKT Tanzania ambayo imetoka kushinda mabao 6-1 dhidi ya Mwadui FC. Djod mwenye bao moja na pasi moja ndani ya Azam FC ambayo imefunga mabao 14 amesema kuwa hawana mashaka kukutana na JKT Tanzania ambayo imetoka kushinda mabao mengi kwenye mechi yao iliyopita. "Hakuna mashaka kukutana na timu ambayo imefunga mabao mengi, ninaona kwamba wao wameshinda mabao 6-1 ilikuwa ni dhidi ya Mwadui na hawakutani na Mwadui kwa sasa wanakutana na Azam FC. "Walikuwa kwenye uwanja mwingine kabisa na hapa wanakuja Uwanja wa Azam Complex hivyo kazi itakuwa ni mpya na sisi tunahitaji kupata ushin

LEO VPL RAUNDI YA NANE INAENDELEA NAMNA HII

Image
  LEO Oktoba 30 safari ya mzunguko wa tisa wa Ligi Kuu Bara unaendelea ndani ya Bongo ambapo mechi mbili zitachezwa kwa timu nne kusaka pointi tatu ndani ya uwanja. Gwambina  iliyo nafasi ya 12 na pointi 9 v KMC iliyo nafasi ya 8 na pointi 10, Uwanja wa Gwambina Complex, saa 10;00 jioni. Azam FC iliyo nafasi ya kwanza na pointi 21 v JKT Tanzania,iliyo nafasi ya 15 na pointi 8 Uwanja wa Azam Complex, saa 1:00 usiku. 

YANGA YAIFUATA BIASHARA UNITED

Image
  KIKOSI cha Yanga leo Oktoba 30 kimeondoka Mwanza kwenda Musoma kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu Bara unaotarajiwa kuchezwa kesho, Oktoba 31. Mchezo huo utachezwa Uwanja wa Karume, Mara utakuwa ni wa nane kwa Yanga huku ukiwa ni wa tisa kwa Biashara United. Timu zote mbili zipo ndani ya tano bora jambo linalomaanisha kwamba zote kwa msimu wa 2020/21 zipo vizuri na zitapambana kupata matokeo ndani ya uwanja. Biashara United ambao ni wenyeji wapo nafasi ya tatu na kibindoni wamekusanya pointi 16 Yanga wapo nafasi ya pili wakiwa na pointi 19. Kwa mujibu wa Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh amesema kuwa wachezaji wote wapo fiti isipokuwa nyota wao Haruna Niyonzima ana sumbuliwa na malaria. Kocha wa Biashara United, Francis Baraza amesema kuwa wapo tayari kwa ajili ya mchezo huo wa kesho.

KUWAONA MASTAA WA SIMBA V MWADUI BUKU TANO TU

Image
 KESHO Oktoba 31, Simba itakuwa na kazi ya kumenyana na Klabu ya Mwadui FC kwenye mchezo wa Ligi huku viingilio ikiwa ni buku 5,(5,000).  Mchezo huo utachezwa Uwanja wa Uhuru saa 10:00 jioni na unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kwa timu zote mbili kutokana na matokeo ya timu hizo mbili. Mwadui FC imetoka kupoteza kwa kufungwa mabao 6-1 dhidi ya JKT Tanzania Uwanja wa Mwadui Complex na Simba imetoka kupoteza kwa kufungwa bao 1-0 dhidi ya Ruvu Shooting, Uwanja wa Uhuru. Ikiwa ni buku 5 kwa mzunguko  VIP B ni shilingi 10,000 na 15,000 kwa VIP A. Kiingilio hicho kitatoa fursa kwa mashabiki kuona uwezo wa nyota wazawa ndani ya Simba inayoongozwa na John Bocco pamoja na uwezo wa kipa namba moja wa Mwadui FC, mzawa Mussa Mbissa.

KUWAONA MASTAA WA SIMBA V MWADUI BUKU TANO TU

Image
 KESHO Oktoba 31, Simba itakuwa na kazi ya kumenyana na Klabu ya Mwadui FC kwenye mchezo wa Ligi huku viingilio ikiwa ni buku 5,(5,000).  Mchezo huo utachezwa Uwanja wa Uhuru saa 10:00 jioni na unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kwa timu zote mbili kutokana na matokeo ya timu hizo mbili. Mwadui FC imetoka kupoteza kwa kufungwa mabao 6-1 dhidi ya JKT Tanzania Uwanja wa Mwadui Complex na Simba imetoka kupoteza kwa kufungwa bao 1-0 dhidi ya Ruvu Shooting, Uwanja wa Uhuru. Ikiwa ni buku 5 kwa mzunguko  VIP B ni shilingi 10,000 na 15,000 kwa VIP A. Kiingilio hicho kitatoa fursa kwa mashabiki kuona uwezo wa nyota wazawa ndani ya Simba inayoongozwa na John Bocco pamoja na uwezo wa kipa namba moja wa Mwadui FC, mzawa Mussa Mbissa.

KOCHA BIASHARA UNITED: WACHEZAJI NIMEWAPA KAZI YA KUPAMBANA NA JEZI YA NJANO

Image
  FRANCIS Baraza, Kocha Mkuu wa Biashara United amesema kuwa amewaambia wachezaji wake wapambane na kila mchezaji atakayekuwa na jezi ya njano uwanjani bila kujali uwezo wake upoje ndani ya uwanja. Kesho, Oktoba 31 Biashara United iliyo nafasi ya tatu kwenye msimamo na pointi 16 itamenyana na Yanga iliyo nafasi ya pili ikiwa na pointi 19. Akizungumza na Saleh Jembe, Baraza amesema kuwa maandalizi ya kikosi yapo vizuri na wanaamini kwamba watapata matokeo kwenye mchezo wa kesho. "Nimewaambia wachezaji kwamba wana jukumu la kuambana na kila mchezaji mwenye jezi ya njano ndani ya uwanja bila kujali uwezo wa wapinzani wangu. "Ni wacheche kwa sasa ambao wamefungwa mabao machache ndani ya ligi ambao ni Yanga sasa kazi kubwa itakuwa kwenye kusaka ushindi hilo lipo wazi lakini tutapambana," amesema. Safu ya ulinzi ya Yanga imeruhusu mabao mawili ya kufungwa ndani ya ligi ikiwa imecheza jumla ya mechi saba huku ile ya Biashara United ikiwa imeruhusu kufungwa mabao s

BAADA YA VICHAPO MFULULIZO SIMBA YAPANIA KUTOFUNGWA

Image
  BAADA ya kupokea vichapo kwenye mechi mbili mfululizo mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara, Simba wamesema kuwa kwa sasa watapambana kutopoteza kwenye mechi zao zijazo ndani ya ligi ili wasifungwe. Simba ilifungwa Oktoba 22 bao 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons, Uwanja wa Nelson Mandela na ilipoteza tena mbele ya Ruvu Shooting, Uwanja wa Uhuru kwa kufungwa bao 1-0. Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara amesema kuwa ili kuweza kufikia malengo yao ya kutwaa ubingwa ni lazima wapate matokeo mazuri hivyo watapambana kwenye mechi zao zijazo. "Bado nina amini kwamba Simba itatatwaa ubingwa kwa msimu wa 2020/21 lakini lazima tupate matokeo mazuri ambayo yatatupa pointi tatu muhimu. "Kushindwa kwetu kwenye mechi zilizopita kunaleta maumivu hivyo mashabiki katika hili wanapaswa wajue kwamba tunahitaji jambo moja ambalo ni umoja na katika umoja wetu Simba hatujawahi kushindwa," amesema. Kesho Oktoba 31, Simba ina kibarua cha kusaka pointi tatu mbele ya Mwadui FC Uwanja wa Uh

NIDHAMU YAIBEBA ARSENAL IKIICHAPA DUNDALK 3-0

Image
MIKEL Arteta,  Kocha Mkuu wa Arsenal amesema kuwa wachezaji wake wameweza kupata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Dundalk kwa sababu walicheza kwa nidhamu.  Mchezo huo wa Europa League uliochezwa Uwanja wa Emirates umeifanya Arsenal kuwa nafasi ya kwanza kwenye msimamo baada ya kufikisha pointi 6 na imefunga jumla ya mabao 5 baada ya kucheza mechi 2 huku Dundalk ikiwa nafasi ya nne na haina pointi kwa kuwa imepoteza mechi zote mbili. Arteta alishuhudia kijana wake Eddie Nketiah dakika ya 42 akipachika bao la kwanza zikiwa zimebaki dakika tatu kabla ya mapumziko huku lile la pili lilipachikwa na Joe Willock dk ya 44 na la tatu dk ya 46 na Nicolas Pepe mabao ambayo yalidumu mpaka mwisho wa mchezo.  Arteta amesema kuwa walicheza kwa nidhamu kubwa jambo ambalo limewapa ushindi wana imani ya kupambana kwa ajili ya mechi zao zijazo ikiwa ni pamoja na ile dhidi ya Manchester United ambayo ni ya Ligi Kuu England itakayochezwa Novemba Mosi.

KMC KAMILI GADO KUVAANA NA GWAMBINA FC

Image
  OFISA Habari wa Klabu ya KMC Christina Mwagala amesema kuwa wapo tayari kwa ajili ya mchezo wa leo Oktoba 30 dhidi ya Gwambina FC. KMC inashuka uwanjani ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza kwa kufungwa mabao 2-1 dhidi ya Yanga kwenye mchezo wao ulioppita uliochezwa Uwanja wa CCM Kirumba. Ikiwa ipo nafasi ya 8 na pointi 11 inakutana na Gwambina FC iliyo nafasi ya 12 na pointi 9 zote zimecheza mechi nane.   Christina amesema:-"Licha ya kupoteza mchezo wa ligi dhidi Yanga, wachezaji wako tayari kuivaa Gwambina ili kupata pointi tatu muhimu. "Maandalizi ya mwisho yamekamilika na wachezaji wote wana  morali nzuri kuelekea katika mchezo huo na lengo ni kuhakikisha kuwa ushindi unapatikana ili kujiweka katika nafasi nzuri kwenye msimamo wa ligi kuu msimu wa 2020/2021. "Kuhusu afya za wachezaji, ziko vizuri na hakuna mchezaji yeyote mwenye majeruhi na kikosi kizima kiko kamili kwa ajili ya mchezo huo hivyo ni jukumu la mwalimu kuona nani ataweza kuwakilisha kwenye mchez

MTIBWA SUGAR HESABU ZAO KWA KAGERA SUGAR, YAANZA SAFARI LEO

Image
  UONGOZI wa Mtibwa Sugar umesema kuwa utapambana kupata matokeo chanya kwenye mchezo wao wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Kagera Sugar utakaopigwa Uwanja wa Kaitaba. Mtibwa inayonolewa na Vincent Barnaba ikiwa imetoka kushinda bao 1-0 dhidi ya Azam FC inakutana na Kagera Sugar iliyotoka kupoteza kwa kufungwa mabao 2-1 dhidi ya Mbeya City City. Ofisa Habari wa Mtibwa Sugar amesema kuwa kikosi kipo tayari kwa ajili ya kupambana na timu yoyote ndani ya uwanja na wana amini watafanya vizuri tofauti na msimu uliopita. "Tulikuwa na msimu mbovu msimu uliopita ila kwa sasa tumeanza kurejea kwenye ule ubora wetu na tunafanya vizuri kwani mambo yanaonekana. "Wale Azam FC walikuwa wanarekodi ya kutofungwa, walizifunga timu nyingi ambazo zilikuwa ndogondogo walipofika kwetu tuliwatuliza na sasa tunaendelea kupambana kwa ajili ya timu nyingine ambazo tutakutana nazo ndani ya uwanja," amesema. Kagera Sugar haijawa na mwendo mzuri ndani ya Kaitaba kwa kuwa ilifungwa pia ilipokutan

BIASHARA UNITED NA YANGA ZAPIGANA MIKWARA

Image
  KIKOSI cha Yanga kilicho nafasi ya pili kwenye msimamo baada ya kucheza mechi 7 na kujikusanyia pointi 19 kitakutana na Biashara United iliyo nafasi ya tatu kwenye msimamo na 16 imecheza mechi 8. Oktoba 31 Yanga ya Cedric Kaze ina kibarua cha kusaka pointi tatu mbele ya Biashara United ya Francis Baraza mchezo utakaochezwa Uwanja wa Karume. Msimu uliopita kwenye mchezo uliowakutanisha wapinzani hawa Uwanja wa Karume ngoma ilikuwa ni 0-0 hivyo kesho kazi itakuwa ngumu kwa timu zote kusaka rekodi mpya ndani ya uwanja huo. Kaze amesema kuwa wachezaji wake wapo tayari kwa ajili ya mchezo huo na anaamini kwamba atapata pointi tatu muhimu. "Mpaka sasa wachezaji wanazidi kuwa imara na imani yangu ni kwamba tutapata pointi tatu kwani nimeona namna kikosi kilivyo na muunganiko umeanza kupatikana,". Baraza amesema kuwa anaamini kwamba anakutana na  timu yenye wachezaji wazuri na uzoefu lakini wachezaji wake wapo tayari kwa mchezo huo watapambana kusaka pointi tatu. &q

SVEN ATAJA SABABU YA KUMPA MAJUKU YA USHAMBULIAJI AJIBU

Image
SVEN Vandenbroeck Kocha Mkuu wa Simba amesema kuwa hakuwa na chaguo la kufanya ndani ya uwanja zaidi ya kumtumia Ibrahim Ajibu kuwa mshambuliaji kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Ruvu Shooting wakati wakipoteza kwa kufungwa bao 1-0. Oktoba 26, Simba ilipokea kichapo cha pili mfululizo ikiwa ni cha pili mfululizo kwa msimu wa 2020/21 baada ya kuanza kufungwa bao 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons. Kwenye mchezo huo Ajibu alipewa jukumu la kusaka ushindi kwa timu yake akilishwa mipira na Luis Miqussone ambaye ana jumla ya pasi tano na bao moja ndani ya ligi. Sven amesema:"Sikuwa na jambo la kufanya kwa kuwa washambuliaji wangu wengi walikuwa ni ni majeruhi hivyo sikuwa na chaguo zaidi ya kumtumia Ajibu kwenye mchezo wetu dhidi ya Ruvu Shooting." Ajibu kwenye mchezo huo alipiga jumla ya mashuti manne ambayo hayakulenga lango. Simba ambao ni mabingwa watetezi kwa sasa wanajiandaa na mchezo wa ligi dhidi ya Mwadui FC utakaochezwa kesho, Oktoba 31 Uwanja wa Uhuru.

AZAM FC YAZITAKA POINTI TATU ZA JKT TANZANIA

Image
  UONGOZI wa Azam FC umesema kuwa utapambana kuendelea na rekodi ya kupata matokeo wakiwa Uwanja wa Azam Complex baada ya kupoteza mchezo wa kwanza kwa kufungwa bao 1-0 dhidi ya Mtibwa Sugar, Uwanja wa Jamhuri, Morogoro. Azam FC inayonolewa na Kocha Mkuu, Aristica Cioaba ilicheza mechi saba bila kupoteza ndani ya ligi ilikutana na balaa la Jaffary Kibaya wa Mtibwa Sugar aliyemtungua David Kissu dakika ya 62 akiwa nje ya 18. Leo Oktoba 30 ina kibarua cha kumenyana na JKT Tanzania iliyo nafasi ya 15 na pointi 8 huku Azam FC ikiwa nafasi ya kwanza na pointi zake 21 zote zikiwa zimecheza mechi 8 ndani ya ligi. Ofisa Habari wa Azam FC, Zakaria Thabit amesema kuwa kupoteza kwao mbele ya Mtibwa Sugar hakujawatoa kwenye reli watarudi kuendeleza rekodi yao mbele ya JKT Tanzania. “Tumepoteza mbele ya Mtibwa Sugar hilo lipo wazi sasa kinachofuata ni kuendelea pale ambapo tulikuwa tumeishia kwa kusaka pointi tatu mbele ya JKT Tanzania kwani utakuwa mchezo wetu tukiwa nyumbani, mashabiki watu

SIMBA: TUNAPITIA KIPINDI KIGUMU KWA SASA

Image
 JONAS Mkude, kiungo mkabaji wa muda mrefu ndani ya Simba ambaye ana uhakika wa namba kikosi cha kwanza amesema kuwa kwa sasa timu hiyo inapitia kwenye kipidi kigumu kutokana na aina ya matokeo ambayo wanayapata. Simba imepoteza mechi mbili mfululizo ndani ya ligi ambazo ni dakika 180 na kuifanya ibaki na pointi zake 13 ikiwa nafasi ya nne kwenye msimamo. Ilipokea kichapo cha kwanza msimu wa 2020/21 mbele ya Tanzania Prisons Uwanja wa Nelson Mandela na ilifungwa bao 1-0 dhidi ya Ruvu Shooting, Uwanja wa Uhuru. Mkude amesema kuwa kutokana na matokeo ambayo wanayapata kwa sasa wapo kwenye kipindi kigumu jambo ambalo wanaliacha mikononi mwa benchi la ufundi. "Matokeo magumu ambayo tunayapata kwetu ni magumu, na tunapitia kipindi kigumu kweli kwa sasa licha ya kupambana kusaka matokeo. "Tukiwa ndani ya uwanja tunacheza kwa juhudi kusaka matokeo ila kinachotokea ni makosa na hapo ninaamini kwamba kocha anaona makosa yetu na anayafanyia kazi. "Ninajua kwamba mash

FOUNTAIN GATE: MALENGO YETU KUSHIRIKI LIGI KUU BARA

Image
 KWA miaka miwili mfululizo tangu 2018, Fountain Gate imefanikiwa kuwa miongoni mwa timu bora zilizofanikiwa kupanda daraja hadi kuweza kushiriki Ligi Daraja la Kwanza msimu huu wa 2020/21 tangu kikosi kuanzishwa. Katika msimu huu ndani ya kundi B, Fountain Gate imeweza kucheza michezo mitatu ambapo alicheza dhidi ya Alliance FC na kufunga mabao 3-0, Rhino Rangers 0-1 na Oktoba 24 Fountain Gate ilicheza dhidi ya Transit Camp na kuweza kufunga mabao 2-0 na kufanikiwa kuipa timu pointi tisa muhimu. Ofisa Habari wa timu hiyo, Juma Ayo amesema kuwa kinachowapa kasi ya mafanikio Fountain Gate ni lengo lao kuu la kutaka kupanda kwenye Ligi Kuu na uwezo mkubwa wa wachezaji waliokuwa nao katika kujielewa wakati wako uwanjani. “Fountain Gate ilianzishwa mwaka 2018 na kiujumla, kinachoifanya Fountain Gate tuwe na kasi ya kupata mafanikio hadi kucheza msimu huu ni kwamba sisi tuna lengo kuu ya kutaka kushiriki katika Ligi Kuu Bara na ndio maana wachezaji wetu wanafanya juu chini katika k

KAZE WA YANGA ATENGEWA MKWANJA WA MAANA KWA AJILI YA KUFANYA USAJILI

Image
  BAADA ya usajili wa kiungo mshambuliaji raia wa Burundi, Said Ntibazonkiza uongozi wa Yanga umesema kuwa upo tayari kufanya usajili mwingine wa mchezaji wa kigeni katika usajili wa dirisha dogo kama Kocha Mkuu Cedric Kaze atapendekeza mchezaji, kwani fedha ipo.   Yanga hivi karibuni ilifanikisha usajili wa Ntibazonkiza baada ya Kaze kupendekeza usajili wake akiwa Canada kabla ya kutua nchini kujiunga na kikosi hicho kilichoweka kambi yake Kijiji cha Avic Town, Kigamboni jijini Dar es Salaam.   Kiungo huyo aliyeitungua Taifa Stars ilipocheza mchezo wake wa kirafiki unaotambulika na Fifa dhidi ya Burundi uliopigwa kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar, anatarajiwa kujiunga rasmi na Yanga Novemba 15, mwaka huu baada ya kumaliza majukumu yake ya timu ya taifa inayowania kufuzu Afcon.   Mkurugenzi Uwekezaji wa GSM na Mjumbe wa Kamati ya Usajili ya Yanga, Injinia Hersi Said alisema kuwa maamuzi yote ya usajili katika dirisha dogo wamemuachia kocha ambaye ndiye atakayesimamia zoezi zima la u

MTUPIAJI NAMBA MOJA NAMUNGO, BLAISE ATAJA KINACHOWAPA TABU

Image
  BIGIRIMANA Blaise, mtupiaji namba moja ndani ya Klabu ya Namungo FC amesema kuwa sababu kubwa inayofanya timu yao kuyumba kwa sasa ni kutokana na uwepo wa maingizo mapya ndani ya timu hiyo jambo linalowapa tabu kupata matokeo. Kwa sasa Namungo FC ikiwa imecheza jumla ya mechi 8 ipo nafasi ya 11 na pointi zake kibindoni ni 10, imeshinda mechi tatu, sare moja na kipigo mechi nne. Blaise ametupia mabao matatu wakati timu yake ikiwa imefunga jumla ya mabao manne ndani ya msimu wa 2020/21 ikiwa chini ya Hitimana Thiery. Nyota huyo ambaye anakipiga pia timu ya Taifa ya Burundi amesema:"Kwa sasa tupo kwenye kipindi cha mpito ukizingatia kwamba wachezaji wengi ni wapya ndani ya kikosi bado kuna wakati unakuja tutafanya vizuri na maisha yatarejea kama ilivyokuwa zamani. "Mashabiki watupe sapoti bado tuna nafasi ya kufanya vizuri na kwa sasa ligi bado ni mbichi, tutafanya vizuri kwenye mechi zetu zijazo," amesema. Mchezo wao ujao ni dhidi ya Dodoma Jiji utakaochezwa

BAKARI MWAMNYETO AMPOTEZA JUMLAJUMLA JOASH ONYANGO WA SIMBA

Image
  BEKI wa kati wa Yanga, Bakari Mwamnyeto ambaye ni mzawa, amempoteza mazima beki kisiki wa Simba,   Joash Onyango   raia wa Uganda kwenye kazi ya ulinzi ndani ya timu hizo mbili ambazo zinatarajiwa kukutana Novemba 7, mwaka huu.   Onyango wa Simba ameshuhudia Aishi Manula akiokota kambani mabao matatu kwenye viwanja vya mikoani ambao alianza kushuhudia kwa mara ya kwanza kwenye Uwanja wa Sokoine wakati Simba ikishinda mabao 2-1 dhidi ya Ihefu.   Kabla hajapoa, Onyango alishuhudia tena Manula akiokota mpira wa pili kwenye nyavu Uwanja wa Jamhuri, Morogoro kwenye sare ya kufungana bao 1-1 na Mtibwa Sugar.   Aliweka lango salama kwenye mchezo dhidi ya Biashara United wakati Simba ikishinda mabao 4-0 Uwanja wa Mkapa na mchezo wa Gwambina wakati Simba ikishinda mabao 3-0.   Uwanja wa Jamhuri, Dodoma akiwa kazini Onyango aliweka lango salama wakati Simba ikishinda mabao 4-0 dhidi ya JKT Tanzania.   Mambo yalikuwa magumu Uwanja wa Nelson Mandela ambapo alimshuhudia Manula akiok