KOCHA MANCHESTER UNITED APATA HOFU KUIKABILI ARSENAL

 


OLE Gunnar Solskajer, Kocha Mkuu wa Manchester United amesema kuwa leo Novemba Mosi ana mtihani mzito wa kusaka pointi tatu mbele ya Arsenal.


Manchester United ambayo imepoteza mechi mbili Uwanja wa Old Trafford mbele ya Crystal Palace na na Tottenham itawakaribisha tena Arsenal saa 1:30 usiku kusaka pointi tatu muhimu.

Arsenal chini ya Kocha Mkuu Mikel Arteta, imeshinda mechi tatu na kupoteza mechi tatu hivyo balaa litakuwa usiku wa leo kwa wababe hawa wawili.


Solskajer amesema:"Kwa Arsenal siku zote kupambana nao sio kazi nyepesi ni wagumu na wanahitaji akili zaidi kwa sababu ni timu nzuri ambayo inaongozwa na kocha mzuri."


Arteta amesema kuwa anaamini utakuwa ni mchezo mgumu lakini ni lazima vijana wake wacheze kwa nidhamu kupata matokeo chanya.



Comments

Popular posts from this blog

SIMBA NA YANGA MSIBEBE MATOKEO UWANJANI

FT: VPL:SIMBA 4-0 IHEFU

WAMEANZA NA MAJANGA MSIMU MPYA WA 2021/22, SIMBA WANAWEZA KUKOSA UBINGWA