MAJEMBE HAYA YA KAZI YAMPA JEURI KOCHA YANGA
K OCHA Mkuu wa Yanga, Juma Mwambusi, amesema kuwa kama atawapata wachezaji wake wote waliokwenda kuzitumikia timu zao za taifa wakiwa salama akiwemo staa Saido Ntibazonkiza na Mukoko Tonombe basi anaamini wataisaidia timu hiyo katika michezo yao inayofuata ya ligi. Wachezaji wa Yanga ambao walikwenda kuzitumikia timu zao za taifa ni pamoja na Saido Ntibazonkiza (Burundi), Tonombe Mukoko (Congo) na Haruna Niyonzima (Rwanda), Feisal Salum, Bakari Mwamnyeto na Deus Kaseke wote kutoka Tanzania. Mwambusi amesema kuwa, hali ya kikosi chake kilichopo kambini ipo sawa kwa wachezaji waliosalia kambini huku akisema kuwa ana matumaini na wachezaji walioenda kuzitumikia timu za taifa wakiwemo Saido, Mukoko Tonombe. Anaamini kuwa ikiwa watare...