Posts

Showing posts from October, 2021

WAMEANZA NA MAJANGA MSIMU MPYA WA 2021/22, SIMBA WANAWEZA KUKOSA UBINGWA

Image
   IKIWA Simba watakuwa kwenye mwendo huu ndani ya msimu wa 2021/22 kengele ya hatari inawaka kwenye kichwa cha Kocha Mkuu, Didier Gomes kwa kuwa kutakuwa na hatihati ya kuachia ubingwa kwa wapinzani wao pamoja na kushindwa kufurukuta kwenye mechi za kimataifa. Hili linakuja kutokana na rekodi kuonyesha kwamba wachezaji wake wengi muhimu wamekuwa wakikutana na minyoosho ya maana huku Gomes akikiri kwamba ligi ni ngumu na ushindani ni mkubwa. Iliwatokea Liverpool ya Ulaya msimu uliopita baada ya kuwakosa nyota wake muhimu kutokana na kupatwa minyoosho uwanjani miongoni mwao alikuwa ni beki kisiki Virgil van Djik ambaye aligongwa na alikaa nje msimu mzima wa 2020/21 na timu yake ikapoteza ubingwa. Hapa Championi Jumatatu inakuletea orodha ya wachezaji walioanza na majanga 2021/22 huku Simba ikiwa ni namba moja kwa timu yenye wachezaji wengi wenye majanga:- Joash Onyango Beki kisiki wa Simba hana bahati na mechi kubwa kwa kuwa aliwahi kupata maumivu kwenye mchezo dhidi ya Kaize

AZAM FC KAMILI GADO KUWAVAA PYRAMID YA MISRI

Image
 MATAJIRI wa Dar es Salaam, Klabu ya Azam FC imeweka wazi kuwa ipo tayari kwa ajili ya mchezo wao wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Pyramid FC ya Misri. Mchezo huo wa kukata na shoka utachezwa bila ya uwepo wa mashabiki kutokana na maelekezo kutoka Shirkisho la Soka Afrika, (Caf) kwa sababu ya suala la Corona. Akizungumza na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa Azam FC, Zakaria Thabit amesema kuwa matarajio makubwa kwa timu hiyo ni kufanya vizuri kwenye kila mchezo ambao watacheza kutokana na uwepo wa wachezaji wazuri pamoja na benchi la ufundi makini. "Azam FC tupo tayari kwa ajili ya ushindani, baada ya kuweza kushinda mechi zile za awali sasa tupo kwenye hatua nyingine ambayo tunatambua kwamba itakuwa ngumu na ushindani ni mkubwa. "Kikubwa ni kuweza kuona tunapata matokeo kwani ipo wazi kila timu ambayo inaingia uwanjani inahitaji ushindi nasi pia tunahitaji kushinda," amesema. Kikosi cha Azam FC kimeendelea na mazoezi kwa ajili ya mchezo huo kwenye viunga vyao pale Azam

KIUNGO YANGA ABAINISHA SABABU ZA KUCHEZA CHINI YA KIWANGO

Image
 KIUNGO mkabaji mpya wa Yanga, Mganda,  Khalid Aucho,amewaambia mashabiki kuwa  watarajie kuona soka safi la pasi linalochezwa  katika baadhi ya klabu kubwa Ulaya kwenye  michezo ijayo wa Ligi Kuu Bara. Kauli hiyo aliitoa mara baada ya mashabiki wa  timu hiyo kulalamikia kiwango kibovu licha ya  kupata ushindi kwenye mechi ya ufunguzi dhidi ya Kagera Sugar. Kwenye mchezo wa kwanza dhidi ya Kagera Sugar ambao ulikuwa ni wa ufunguzi kwa msimu wa 2021/22 Yanga ilifanikiwa kupata  ushindi wa bao 1-0 lililofungwa na kiungo mzawa, Feisal Salum ‘Fei Toto’ kwa shuti kali ndani ya  18 Uwanja wa Kaitaba.  Nyota huyo alisema kuwa kwenye mechi yao dhidi ya Kagera Sugar walicheza wakiwa wamechoka baada ya kutumia nguvu mbele ya Simba lakini wana imani ya kuendelea kufanya vizuri kwenye mechi zijazo.  "Mchezo wetu dhidi ya Kagera ulikuwa mgumu, lakini licha ya ugumu tunashukuru kuanza ligi  vizuri kwa ushindi ambao umetuongezea nguvu  katika michezo ijayo. “Mchezo wa mwanzo tulicheza

ORODHA YA NYOTA WANAOMPASUA KICHWA GOMES,KUNA KESI MAALUMU

Image
  LAZIMA kichwa cha Didier Gomes kwa sasa kiwe kinapasuka kwa sababu mastaa wake wote nao ni pasua kichwa kutokana na mwendo wao ulivyo pamoja na mechi ambazo zipo mbele yake. Gomes anakibarua cha kutetea taji la Ligi Kuu Bara ambalo Simba ilitwaa msimu uliopita wa 2020/21 pia ana kazi ya kuhakikisha kikosi hicho kinaweza kutinga hatua ya robo fainali Ligi ya Mabingwa na zaidi ya hatua hiyo ila sasa mastaa wake wameanza tofauti kabisa msimu huu. Hii ni alama mbaya ikiwa hali itaendelea kuwa namna hii na majanga yakaendelea lazima Gomes achange karata vizuri huku akivuta picha kwamba kwa sasa hana nyota wake wawili ambao ni Clatous Chama na Luis Miquissone waliokuwa ni wachezaji muhimu pia kikosi cha kwanza. Spoti Xtra ilipata nafasi ya kuzungumza na Gomes ili kujua kuhusu hesabu zake pamoja na namna ambavyo anawatazama wachezaji wake hao ilikuwa namna hii:- Sadio Kanoute Nyota huyu ingizo jipya ndani ya kikosi cha Simba mwenye umri wa miaka 24 ni raia wa Mali na alitambuli

JEZI AMBAZO ZILISTAAFISHWA NA SABABU PIA

Image
 KUNA namba za jezi ambazo huwa zinastaafishwa na kuwekwa kabatini mazima huko majuu Kibongobongo huwa inakuja kisha inakataa lakini leo acha tucheki zile za mbele kwanza namba za jezi ambazo zilistaafishwa kutokana na sababu mbalimbali. Kwa timu ya Birmingham City jezi namba 22 iliwekwa kabatini na hakuna mchezaji ambaye atakuja kuitupia tena na sababu ya jezi hiyo kustaafishwa ni baada ya Birmingham kuwapa heshima ya kuvunja rekodi ya uhamisho klabuni hapo wakimuuza kiungo wao Jude Bellingham kwenda Klabu ya Borussia Dortmund kwa pauni milioni 25. Namba 10 2000 Klabu ya Napoli walikubali kuistaafisha jezi namba 10 iliyokuwa ikivaliwa na legend, Diego Maradona na hiyo ilikuwa ni kutokana na mchango wa nyota huyo aliyedumu miaka 7 katika timu hiyo. Aliweza kutimiza majukumu kwa timu yake kutwaa taji la Serie A mara mbili ambayo wanayo mpaka sasa. Timu ya taifa ya Argentina ilitaka kufanya hivyo mwaka 2020 ila Shirikisho la Soka la Kimataifa, (Fifa) liliweka ngumu. Kwa sasa nyo

ORODHA YA MASTAA WANAOPIGIWA HESABU NA NEWCASTLE

Image
KLABU ya Newcastle United inatajwa kuanza kuandaa orodha ya mastaa wakubwa ambao watakuwa ndani ya timu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu England. Hivi karibuni klabu hiyo imenunuliwa na matajiri wakubwa akiwemo Mohammed bin Salman na Simon Brothers inaonyesha kuwa inataka kushusha majembe kadhaa ya maana kwenye ligi. Kuna nyota kibao wakubwa wamekuwa wakitajwa kwamba wanaweza kuibuka katika kikosi hicho kutokana na uwepo wa mkwanja wa kutosha kwa mabosi hao wapya. Mastaa ambao wanatajwa kuwekwa kwenye rada za timu hiyo ni pamoja na Gareth Bale, Edinson Cavani, Neymar Jr na Mauro Icard. Pia jina la Steven Gerrad ambaye anaifundisha Rangers ya Scotland linatajwa kuwa kwenye orodha ya makocha ambao wanaweza kuinoa timu hiyo. 

VIDEO:TAZAMA NAMNA WANAJESHI WA MPAKANI WANAVYOWAVUTIA KASI AL AHLY TRIPOL

Image
BIASHARA united wanajiita Wanajeshi wa Mpakani wana kibarua cha kusaka ushindi kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Al Ahly Tripol ya Libya unaotarajiwa kuchezwa kesho, Oktoba 15 Uwanja wa Mkapa.  Wachezaji hao wameendelea kuwavutia kasi wapinzani wao kwa kufanya mazoezi Uwanja wa Mkapa.Miongoni mwa nyota hao ni pamoja na Duchu,Redondo,James Ssetuba ambao wapo Dar kwa ajili ya maandalizi ya mchezo huo.  

RONALDO AMPIKU MESSI KWENYE SUALA LA HATTRICK

Image
 WABABE wawili kwenye ulimwengu wa soka bado wanakimbizana kwenye ishu ya kuandika rekodi ambapo kila mmoja anazidi kupambana kuweka mambo sawa. Ukitaja wachezaji wawili ambao wanatawala soka la dunia kwa zama za sasa ikiwa ni katika kipindi cha miaka 12 huwezi kuacha kumtaja Cristiano Ronaldo raia wa Ureno na Lionel Messi mwamba raia wa Argentina. Wachezaji hawa wameweza kuchukua Ballon d’or 11 wote wawili idadi kubwa kwao ambapo katika hili mbabe alikuwa ni Messi ambaye amechukua tuzo hiyo kubwa mara 6 na Cristiano akichukua mara 5. Katika kipindi ambacho Messi aliweza kusepa na tuzo hiyo ya Ballon d’0r  alikuwa ndani ya Klabu ya Barcelona  na Cristiano yeye amepata mafanikio akiwa anatumika klabu tofautitofauti ikiwa ni pamoja na Manchester United, Juventus na Real Madrid. Kwenye kitengo cha kufunga  Hatrick hapa Ronaldo kampoteza mazima Messi ambapo jumla Ronaldo amefunga hat trick 58 huku mshikaji wake Messi akiwa na hat trick 55. Toafuti yao hapa ni tatu pekee lakini kw

KUNA UWEZEKANO TIMU ZIKABORONGA KIMATAIFA,KAZI NI NGUMU

Image
  UWEZEKANO ni mkubwa kwa sasa timu zetu zikaboronga kwenye mashindano ya kimataifa ikiwa hazitajipanga vizuri kutokana na mambo kubadilika kila iitwapo leo. Tunaona kwamba ni timu tatu ambazo zinatoka Tanzania zimebaki kwenye mashindano ya kimataifa kuondoka kwa mmoja ni pigo ambalo linapaswa kuzibwa na hawa waliopo nao pia wapo kwenye mazingira magumu kwa sasa. Yanga ambao walikuwa pia katika kuipeperusha bendera ya Tanzania haikuwa bahati kwao licha ya kupambana kusaka matokeo pamoja na mpango wa kuitangaza Tanzania kupitia jezi yao ya mashindano ya kimataifa. Ukianza kutazama kwenye Ligi ya Mabingwa haya mashindano ambayo ni makubwa kwa hadhi ndani ya bara la Afrika ni Klabu ya Simba imebaki kupambana kwa ajili ya kupata matokeo. Hapa kazi ni kubwa tofauti na msimu uliopita kwa kuwa kile kikosi cha dhahabu cha Simba kimemeguka na kilichobaki kwa sasa ni kile ambacho kinaundwa kwa mara nyingine. Haina maana kwamba kikosi cha Simba kwa sasa sio bora hapana ukweli ni kwamba ki

SIMULIZI YA FAMILIA ILIYOKUWA NA MIGOGORO YA MARA KWA MARA

Image
SIMULIZI ya familia iliyokuwa na migogoro ya mara kwa mara Ndugu wanapaswa kuishi kwa amani kwa wakati wowote ule. Hili lilikuwa ni tofauti kabisa  katika familia ya upande wa mume wangu kwani ndugu wote wanne waliishi kuwa wenye ugomvi kila  mara huku tusijue kile walichokuwa wakizozania kwa wakati ule.  Nilidhania kwa wakati  mwingine waligombania shamba lakini hili lilikuwa tofauti kabisa na kila mtu alikuwa amesha pewa mgao wake wa shamba kwa usawa.  M ali ambayo babayao aliwaachia nyuma baada ya  kufariki walikuwa wameigawanya kwa usawa na hakuna hata yeyote aliyeachwa nyuma ama  kutengwa kwa wakati wowote ule.  Sikujua chanzo haswa cha ugomvi baina yao.Hali ile  ilipelekea hata mume wangu kutishiwa maisha yake na baadhi ya ndugu zake. Hakufahamu fika  ni kwanini walitaka kumwangamiza licha yake kuwa ndugu wao wa toka nitoke. Siku zilivyosonga ndipo mambo yalizidi kuwa magumu zaidi. Hapo awali walikuwa wakikutana  kwenye mikutano ya familia na kuzungumza mambo yaliyowasum

BOSI PSG ATAKA MADRID WAPEWE ADHABU KUBWA

Image
 MKURUGENZI wa masuala ya michezo ndani ya Klabu ya PSG, Leonardo Araujo amesema kuwa Klabu ya Real Madrid inapaswa kupewa adhabu kubwa. Imekuwa ikielezwa kuwa Madrid wanahitaji saini ya mshambuliaji wa PSG Kylian Mbappe ambaye bado ni mali ya timu ya PSG inayoshiriki Ligue 1 hivyo kitendo cha kuripotiwa kwamba amefanya mazungumzo na timu inayohitaji saini yake ni kinyume na utaratibu kwa kuwa bado ana mkataba na timu yake ya sasa. Kiongozi huyo amesema kuwa Madrid walionyesha kutokuwa na nidhamu kwa PSG pamoja na soka kiujumla kutokana ana kuzungumza kuhusu mchezaji wa timu nyingine. Mbappe mwenyewe aliwahi kusema kuwa anataka kuondoka PSG ili akapate changamoto mpya na timu ambayo anatajwa kwenda ni Madrid ambao wanatajwa kuwa wamekuwa wakimshawishi afanye hivyo jambo ambalo limewakasirisha mabosi wa PSG. Taarifa imesema kuwa Madrid wapo tayari kutoa kitita cha Euro milioni 200 kwa ajili ya mchezaji huyo kinda raia wa Ufaransa. "Nafikiri Madrid wanatakiwa kupewa adhabu kw

VIDEO:HILI HAPA BASI JIPYA LA YANGA MUONEKANO WAKE

Image
IKIWA ni msimu mpya wa 2021/22 mambo ni mapya pia kwa mabingwa mara 27 wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga ambao nao pia wana basi jipya kwa ajili ya msimu mpya ni Marcopolo chapa kama zote na wanalitumia kwa ajili ya usafiri wa wachezaji pamoja na viongozi, huu hapa muonekano wake kwa nje.  

BIASHARA UNITED YAWAVUTIA KASI AL AHLY TRIPOLI

Image
  WANAJESHI wa mpakani, Biashara United,  leo Oktoba 13 wameendelea kuwavutia kasi wapinzani wao katika mchezo wa Kombe la Shirikisho unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa. Itakuwa ni Oktoba 15, Ijumaa dhidi ya Al Ahly Tripoli ya Libya na ule wa marudio unatarajiwa kuchezwa nchini Libya. Wachezaji wote wapo tayari kwa ajili ya mchezo huo ambao unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa. Miongoni mwa mastaa ambao walikuwepo mazoezini leo ni pamoja na Redondo, kipa namba moja James Ssetuba, Duchu. Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Biashara United,  Seleman Mataso amesema kuwa wapo tayari kwa ajili ya kupata matokeo chanya.

AZAM FC KUJA NA JAMBO HILI KUBWA

Image
MABOSI wa Azam FC wameamua kuwa karibu na mashabiki wao ambapo siku ya mchezo wao wa kimataifa dhidi ya Pramids ya Misri wataweka bonge moja ya screen nje. Taarifa rasmi iliyotolewa na Azam FC imeeleza:"  Siku zote tunawajali mashabiki wetu, sasa mtaweza kushuhudia mchezo wetu wa raundi ya kwanza ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Pyramids ya Misri, kwenye luninga kubwa tutakayoifunga nje ya Uwanja wa Azam Complex Jumamosi hii saa 9.00 Alasiri. "Wakati unashuhudia mbungi hiyo ya viwango, utaweza kupoza koo lako kwa kujipatia viburudisho murua kabisa kutoka Officialbakhersagroup  kama vile Maji ya Uhai, Mango Crush, Azam Ice Cream, Azam Ukwaju, Azam Energy, Azam Cola, Juisi za African Fruti, Apple Punch. "Azam FC tunazidi kuwakumbusha kuwa mchezo huo hautakuwa na mashabiki, watakaoruhusiwa kuingia ndani ya uwanja tukitekeleza agizo kutoka Shirikisho la Soka Afrika (CAF),"

GOMES AJIVUNIA UWEPO WA JEMBE HILI LA KAZI SIMBA

Image
 KOCHA Mkuu wa Simba Didier Gomes amesema kuwa anamtambua vema mshambuliaji wake Kibu Denis hivyo ana uhakika kwamba atakuja kuwa mchezaji muhimu kwenye timu hiyo. Kwa sasa Simba inafanya maandalizi ya mwisho kuelekea kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Jwaneng Galaxy ya Botswana. Akizungumza na Saleh Jembe, Gomes amesema kuwa kwa namna ambavyo amemtazama Kibu akiwa kwenye timu ya taifa na muda aliokuwa nao kwenye mazoezi ni jambo ambalo linampa matumaini kwamba atafanya vizuri. Nyota huyo ni ingizo jipya ndani ya Simba ambapo aliibuka hapo akitokea kikosi cha Mbeya City kwa dili la miaka miwili. Gomes amesema:"Kibu ni moja ya wachezaji wazuri na amekuwa kwenye mwendo mzuri katika kutimiza majukumu yake niliweza kumuona kwenye mechi ambazo tulicheza alikuwa vizuri. "Hata kwenye mchezo wa timu ya taifa dhidi ya Benin nimeona kwamba ana kitu ambacho amekionyesha hivyo nina amini kwamba atakuja kuwa mchezaji muhimu kwenye kikosi," amesema.  Simba itaku

YANGA YATENGA SIKU TISA ZA USHINDI NDANI YA LIGI KUU BARA

Image
 KOCHA Mkuu wa Yanga, Nasreddine Nabi, amepanga kwamba, baada ya mchezo wao wa Ligi Kuu Bara dhidi ya KMC utakaochezwa Oktoba 19, mwaka huu, atatumia takribani siku tisa kukijenga kikosi chake kuimaliza Azam FC. Katika maandalizi hayo ya siku tisa kuiwinda Azam, Yanga inatarajiwa kucheza mchezo mmoja wa kirafiki dhidi ya timu kutoka Kenya kati ya Sofapaka au Tusker. Kabla ya hapo, Jumapili, Yanga ikicheza mechi ya kirafiki dhidi ya JKU ya Zanzibar kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar. Katika mchezo huo Yanga ilishinda bao 1-0 na mtupiaji alikuwa ni Fiston Mayele ambaye alipachika bao hilo kipindi cha kwanza lilidumu mpaka dakika 90 zilipokamilika.   Chanzo kutoka ndani ya Yanga, kimeliambia Spoti Xtra kuwa: “Kocha Nabi hataki masihara kabisa na timu yake kwani baada ya mechi ya Ngao ya Jamii dhidi ya Simba, aliomba siku 30 kwa ajili ya kuimarisha kikosi chake cha msimu huu. “Kwa sasa ndicho anachokifanya kwani baada ya timu kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya JKU ya Zanzibar, hesabu ni

VIDEO:TAZAMA WANAJESHI WA MPAKANI WALIVYOWASILI NA NDINGA YAO KWA MKAPA

Image
MASTAA wa Biashara United leo Oktoba 13 walikuwa na kazi ya kufanya Uwanja wa Mkapa ikiwa ni maandalizi ya mechi yao ya kimataifa dhidi ya Al Ahly Tripol ya Libya unaotarajiwa kuchezwa Oktoba 15, Uwanja wa Mkapa.  Wanajeshi hao wa mpakani waliwasili namna hii Uwanja wa Mkapa na ndinga yao.   

MBINU ZA WABOTSWANA MIKONONI MWA GOMES

Image
 IMEBAINISHWA kuwa, video za mechi za wapinzani wa Simba katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika, Jwaneng Galaxy, zitaamua aina ya kikosi ambacho kitaanza kwenye mchezo unaotarajiwa kuchezwa Oktoba 17, mwaka huu. Habari kutoka Benchi la Ufundi la Simba, zimeeleza kuwa, baada ya Kocha Mkuu, Didier Gomes kupata video za wapinzani wao, walikaa kikao kujadili namna ya kuwakabili. Kupata video hizo ni sawa na kupata mbinu za wapinzani hao ambao watakutana na Simba kwenye mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkali. “Haikuwa kazi rahisi kupata video zao za hivi karibuni kwani inaonekana hawajacheza muda mrefu, lakini kwa zile ambazo zimepatikana zilitazamwa kwa umakini na baada ya kutazamwa kikao ilibidi kifanyike kuwajadili wapinzani wetu. “Kikao hicho kiliamua aina ya wachezaji ambao wataanza kwenye mchezo ujao ila kwa sasa ambacho kinatazamwa ni kurejea kwa wachezaji kutoka kwenye majukumu yao ya timu za taifa pamoja na wale ambao ni majeruhi,” ilieleza taarifa hiyo. Kuhusu wap

VIDEO:TAZAMA MUONEKANO WA UWANJA WA MKAPA NYAKATI USIKU

Image
UWANJA wa Mkapa uliopo Temeke ni moja ya viwanja bora Afrika Mashariki na kati na ni sehemu pia ambayo wageni wengi hufika na kujionea burudani mbalimbali.Huu hapa ni muonekano wake nyakati za usiku.   

KIPA MPYA SIMBA MAMBO BADO

Image
DIDIER Gomes, Kocha Mkuu wa Simba amesema kuwa kipa wake Jeremia Kisubi bado anahitaji muda ili kuweza kufanya vizuri. Kisubi kwa sasa yupo ndani ya kikosi hicho ambacho kinafanya maandalizi ya mwisho kuelekea kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Jwaneng Galaxy ya Botswana. Gomes amesema anatambua uwezo wa nyota huyo na amekuwa akifanya vizuri kwenye mazoezi lakini bado kuweza kuanza katika kikosi cha kwanza kwa kuwa hajawa imara. "Kisubi ni kipa mzuri lakini bado hajawa imara kwa sasa kwa sababu alikuwa anaumwa kwa muda mefu na wakati huu anaendelea na mazoezi. "Jambo ambalo linasubiriwa kwake ni kuwa katika hali yake ya kawaida na hiyo itafanya tuwe na chaguo kubwa kwenye upande wa makipa,".

WANACHOKITAKA MASTAA YANGA NI HIKI HAPA MBALI NA MKWANJA

Image
 ACHANA na bonasi za kila mechi wanazozipata kutoka kwa wadhamini wao kampuni ya GSM imefichuka kuwa kitu kikubwa ambacho kinawapa motisha ya kufanya vizuri mastaa wa Yanga, ni malengo ya kutaka kuandika rekodi ya kushinda ubingwa wa Ligi Kuu Bara baada ya kupita misimu minne. Yanga imeuanza kwa kasi msimu huu wa 2021/22 kwa kushinda taji la Ngao ya Jamii na kuvuna pointi sita katika michezo yao miwili ya kwanza, huku wakiwa nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara mpaka sasa.  Mara ya mwisho Yanga kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara ilikuwa msimu wa 2016/17, na baada ya hapo Simba walitwaa taji hilo mara nne mfululizo. Akizungumza na Championi Jumatatu, aliyekuwa Kaimu Katibu Mkuu ambaye sasa ni Mkurugenzi wa fedha wa Yanga, Haji Mfikirwa alisema: “Miongoni mwa sera za klabu yetu katika kuwapa motisha wachezaji ni kuhakikisha kunakuwepo na kiwango fulani cha bonasi kwa kila matokeo mazuri wanayoyapata. "Lakini nikuhakikishie kuwa hicho siyo kitu pekee kinachowapa motisha

VIDEO:YANGA YAPIGWA RUNGU CAF, SIMBA YASAFIRISHA MPISHI BOTSWANA

Image
SHIRIKISHO la Soka Afrika, (CAF) limeipiga rungu Yanga kutokana na kukiuka taratibu kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Rivers United, Simba wasafirisha mpishi Botswana.   

SIMULIZI YA MFANYABIASHARA ALIYEFANIKIWA KUIMARISHA BIASHARA YAKE

Image
SIMULIZI ya aliyeimarisha biashara yake  Ni lengo la kila mfanyabiashara kuona biashara yake inanawiri. Bishara inapoenda chini kwa  wakati wowote humfanya mwenyewe kukosa imani na kazi ile na hata mara nyingi anaweza  kuifunga na kujishugulisha na mambo ambayo yanaweza kumpatia kipato kando na biashara. Niliishi mjini Nakuru ambapo nilikuwa nimefungua kibanda kidogo kwenye steji ya magari  mjini Nakuru. Kando na kuwa kibanda ilikuwa ni kijihoteli kidogo ambapo lengo langu lilikuwa  kupata madereva na abiria wa magari waliotaka kula lakini mambo yaliniendea mrama kwani kwa  siku nilirudi nyumbani bila hata ya kufikisha faida niliyokuwa natarajia.  Wahudumu hawa  walienda kwenye migahawa ya wafanyibiashara wengine. Hali hii ilifanya vyakula vyangu  kuharibika na mara kwa mara nilikuwa navimwaga kila mara.  Hii haikuninifanya mimi  kukata tamaa kwani niliendelea na biashara ile kwa matumaini kuwa hapo mwishowe bahati  itaanguka upande wangu. Mara kwa mara wateja walipita biashara

BIASHARA UNITED HALI NI TETE,HAKUNA TIKETI ZA KIMATAIFA

Image
  UONGOZI wa Biashara United umeweka wazi kuwa kwa sasa vichwa vinawauma kuhusu suala la usafiri wa wachezaji wao kuelekea nchini Libya kwa ajili ya mchezo wa kimataifa wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Al Ahly Tripoli. Biashara United ina kibarua cha kusaka ushindi katika mchezo wa Kombe la Shirikisho raundi ya kwanza dhidi ya Al Ahly Tripoli ya Libya ambao unatarajiwa kuchezwa Oktoba 15, Uwanja wa Mkapa. Seleman Mataso, Mwenyekiti wa Biashara United amesema kuwa kuhusu mchezo wao wa nyumbani hawana tatizo ila kinachowaumiza ni ule wa marudio nchini Libya hali ni mbaya. Akizungumza na Saleh Jembe, Mataso alibainisha kuwa wanahitaji kufanya vizuri kimataifa ila hali ni tete kwenye upande wa mkwanja. “Hali ni mbaya sana kwa ajili ya mchezo wetu wa marudio ugenini, kwa muda huu gharama za matumizi ya safari mambo hayajakaa sawa na hata tiketi pia bado hatujapata hivyo wadau watupe sapoti katika hili,” . Biashara United inayonolewa na Kocha Mkuu Patrick Odhhiambo iliweza kufika kati

YUSUPH ATHUMAN WA YANGA ANAHITAJI KUFUNGA MABAO YAKUTOSHA

Image
 MSHAMBULIAJI mpya wa Yanga, Yusuph Athumani amesema kuwa anahitaji kupambana kuhakikisha anafunga mabao ya kutosha ili yamfanye awe anapata nafasi ya kucheza mara kwa mara katika kikosi cha kwanza cha Yanga. Yusuph Athumani ambaye amejiunga na Yanga katika dirisha kubwa lililopita la usajili anapata upinzani mkali wa kuanza katika kikosi cha kwanza mbele ya washambuliaji wenye uraia wa DR Congo, Fiston Mayele na Heriter Makambo. Akizungumza na Championi Jumatatu, Yusuph alisema kuwa anahitaji kufunga mabao ya kutosha pindi anapopata nafasi ya kucheza kwani anaamini akifanya hivyo atamshawishi kocha kumpa nafasi ya kucheza mara kwa mara ndani ya kikosi cha kwanza cha timu hiyo. “Hakuna njia nyingine ya mimi kuweza kupata nafasi ya kucheza mara kwa mara kama kufunga,malengo yangu ni hayo ni kufunga katika nafasi ambayo nipata yakucheza hiyo naamini itamshawishi mwalimu kunipatia nafasi mara kwa mara. “Ushindani wa namba ni mkubwa lakini naamini kila mchezaji atacheza kwa wakati

ISHU YA FAINI KUTOKA CAF, YANGA YAGOMEA YAKATA RUFAA

Image
  SHIRIKISHO la Soka Afrika, (Caf) limeipiga rungu ya faini ya milioni 11 Yanga kutokana na kile kilichoelezwa kuwa kufanya fujo kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Rivers United pamoja na kuingiza mashabiki kwenye mchezo huo. Ikumbukwe kwamba Septemba 12, Uwanja wa Mkapa baada ya dakika 90 kwenye mchezo wa awali ubao ulisoma Yanga 0-1  Rivers United, ilielezwa kuwa wapinzani hao wa Yanga walipeleka malalamiko Caf kuwa walifanyiwa vurugu pamoja na uwepo wa mashabiki kwenye mchezo ambao haukupaswa kuwa na mashabiki. Taarifa kutoka Caf imeeleza kuwa Yanga walishindwa kujibu taarifa za tuhuma hizo za kuwafanyia fujo watu waliokuwa kwenye msafara wa Rivers United ya Nigeria pamoja na kubaini uwepo wa mashabiki uwanjani. Akizungumza na Championi Jumatano,Mkuu wa Idara ya Habari wa Yanga, Hassan Bumbuli aliweka wazi kuwa walipata barua hiyo ila wameshangazwa na hukumu hiyo jambo ambalo limewafanya wakate rufaa. “Tulipokea barua Oktoba 5 na tulipaswa kuijibu, kabla hatuja

MWAMBA POGBA MABAO YAKE KAMA MIAKA YAKE

Image
 WAKATI timu yake ya taifa ya Ufaransa ikifanikiwa kutwaa taji la UEFA Nations League kwa mara ya kwanza katika historia nyota Paul Pogba bado ni wa moto katika rekodi akiwa uwanjani katika mechi za Premier League. Ikumbukwe kwamba Ufaransa ilitwaa taji hilo baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Hispania ambapo mabao yalifungwa na Kylian Mbappe pamoja na Karim Benzema na Pogba pia alikuwa sehemu ya kikosi cha ushindi. Kiungo huyo mwenye miaka 28 aliletwa duniani Machi 15, 1993 anapenda kuvaa jezi namba 6 akiwa na timu yake ya Manchester United inayonolewa na Kocha Mkuu, Ole Gunnar Solskjaer. Mpaka sasa ndani ya Manchester United ambapo aliibukia hapo 2016 akitokea Klabu ya Juventus amecheza jumla ya mechi 144 za ushindani. Alipokuwa Juventus msimu wa 2012/2016 aliweza kucheza jumla ya mechi 124 na alitupia mabao 28 kama umri wake wa sasa. Weka kando ishu za Juventus sasa tunarudi katika Klabu ya Manchester United ambapo yupo kwa sasa huku dili lake nalo likizidi kuyeyuka t

TAWI JIPYA LA AZAM FC LAZINDULIWA NA BASI JIPYA

Image
WAKIWA na basi jipya ambalo wanaliita ndege ya ardhini, Azam FC wamezindua pia tawi jipya na limepewa jina la Ofisa Habari wa Azam FC, Zakaria Thabit, Zaka Zakazi. Habari inasema kwamba ni basi jipya la Azam FC kwa msimu wa 2021/22 limezindua tawi hilo kwa mujibu wa taarifa iliyoandikwa kwenye kibao cha tawi hilo jipya. Ofisa Habari wa Azam FC, Zakazakazi ameshukuru kwa hilo lililotokea kwa jina lake kuwakilisha tawi la mashabiki wa Azam FC. Zakazi amesema:"Asanteni sana wanangu wa Mbande kwa heshima hii. Tuko pamoja,".  

RONALDO AFIKISHA JUMLA YA HAT TRICK 58

Image
MSHAMBULIAJI wa timu ya taifa ya Ureno,   Cristiano Ronaldo ameweka rekodi ya kufunga jumla ya hat trick 58 katika maisha yake ya mpira baada ya kutupia kwenye mchezo wa kuwania kufuzu Kombe la Dunia mbele ya Luxembourg.  Kwenye mchezo huo wa kuwania kufuzu Kombe la Dunia ikiwa ni kundi A, ubao wa Uwanja wa Algarve ulisoma Ureno 5-0 Luxembourg na kufanya Ureno kufikisha jumla ya pointi 16 ikiwa nafasi ya pili na vinara wa kundi hilo ni Serbia wenye pointi 17. Ronaldo alitupia mabao mawili kwa penalti ambapo ilikuwa ni dakika ya 8 na 13 na lile la kukamilisha hat trick ilikuwa ni dakika ya 87 akilipachika kwa kichwa na yale mengine mawili yalitupiwa na Bruno Fernandes dakika ya 17 na Joao Palhinha dakika ya 69.  Kwenye mchezo huo Ureno walipiga jumla ya mashuti 21 na ni mashuti 11 yalilenga lango huku wapinzani wao wakipiga mashuti matatu pekee na ni mashuti mawili yaliweza kulenga lango ila hayakubadilika kuwa bao.