ORODHA YA MASTAA WANAOPIGIWA HESABU NA NEWCASTLE


KLABU ya Newcastle United inatajwa kuanza kuandaa orodha ya mastaa wakubwa ambao watakuwa ndani ya timu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu England.

Hivi karibuni klabu hiyo imenunuliwa na matajiri wakubwa akiwemo Mohammed bin Salman na Simon Brothers inaonyesha kuwa inataka kushusha majembe kadhaa ya maana kwenye ligi.

Kuna nyota kibao wakubwa wamekuwa wakitajwa kwamba wanaweza kuibuka katika kikosi hicho kutokana na uwepo wa mkwanja wa kutosha kwa mabosi hao wapya.

Mastaa ambao wanatajwa kuwekwa kwenye rada za timu hiyo ni pamoja na Gareth Bale, Edinson Cavani, Neymar Jr na Mauro Icard.

Pia jina la Steven Gerrad ambaye anaifundisha Rangers ya Scotland linatajwa kuwa kwenye orodha ya makocha ambao wanaweza kuinoa timu hiyo. 


Comments

Popular posts from this blog

SIMBA NA YANGA MSIBEBE MATOKEO UWANJANI

FT: VPL:SIMBA 4-0 IHEFU

WAMEANZA NA MAJANGA MSIMU MPYA WA 2021/22, SIMBA WANAWEZA KUKOSA UBINGWA