Posts

Showing posts from December, 2020

NYOTA WA SIMBA CHAMA MIKONONI MWA YANGA

Image
  MEFAHAMIKA kuwa, Yanga imemalizana kwa siri na kiungo mchezeshaji wa Simba, Mzambia, Clatous Chama huku ikimfanyia kufuru kubwa nyota huyo. Mzambia huyo ambaye ni kipenzi cha Simba, kama kila kitu kitaenda sawa, basi atatua kuichezea Yanga kuanzia msimu ujao ikiwa ni baada ya mkataba wake wa miaka miwili ndani ya Simba kumalizika.   Kiungo huyo alikuwa kwenye mipango ya muda mrefu ya kusajiliwa na Yanga ikiwemo katika usajili mkubwa msimu huu, lakini mkataba wake ndiyo ulizuia mipango hiyo kukamilika. Kwa mujibu wa taarifa ambazo imezipata Spoti Xtra, Kampuni ya GSM ambao ndiyo wanaofanikisha usajili Yanga, wamefanya kufuru kubwa Chama ya kumjenga nyumba ya kisasa na kifahari nyumbani kwao Zambia.   Mtoa taarifa huyo alisema kuwa, GSM imemjengea nyumba kiungo huyo katika sehemu ya masharti aliyowapa matajiri hao huku akiomba dau kubwa la usajili ambalo huenda likaweka rekodi. Aliongeza kuwa, pia kiungo huyo ameahidiwa gari la kutembelea la kifahari atakalolitumia katika ma

OLE GUNANAR ATAMBA KUENDELEZA DOZI

Image
  KOCHA Mkuu wa Manchester United, Ole Gunnar Solskjaer, amesema kuwa anaamini timu yake inaweza kuifunga timu yoyote kwa sasa.   Manchester United wamekuwa wakionesha kiwango cha juu kwa siku za hivi karibuni na sasa wanashika nafasi ya pili kwenye Ligi Kuu England.   United ilifanikiwa kuichapa Wolves bao 1-0 na kuendelea kufanya vizuri kwenye michezo ya ligi hiyo ikiwa inaufukuzia ubingwa kwa sasa baada ya kucheza michezo 15.   Solskjaer amesema:"Haya matokeo ni bora sana kwetu, Man United kwa sasa ina morali ya hali ya juu na hicho ndicho kinasaidia. “Kwa sasa tupo tofauti, wachezaji wanaamini wanaweza kumfunga yeyote.   "Ni mapema sana kusema kuhusu ubingwa kwa kuwa tumecheza michezo 15 tu, ni jambo ambalo tunaweza kulifikiria kuanzia Machi mwakani,” amesema Solskjaer. Ipo nafasi ya pili kwenye msimamo ikiwa na pointi 30 kinara ni Liverpool mwenye pointi 33. Leo United inacheza na Aston Villa, Uwanja wa Old Trafford.

ISHU YA MEDDIE KAGERE NA KOCHA MKUU SIMBA IMEKAA HIVI

Image
  KOCHA Mkuu wa Simba, Sven Vandenbroeck amesema kuwa hana tatizo na mshambuliaji namba moja wa kikosi hicho Meddie Kagere. Imekuwa ikielezwa kuwa Sven na Kagere hawaivi chungu kimoja jambo ambalo lilikuwa likimfanya amsotesha benchi nyota huyo ndani ya kikosi cha Simba. Tayari kwa sasa ameanza kumtumia nyota huyo ambaye ametupia jumla ya mabao saba ndani ya Ligi Kuu Bara kwa msimu wa 2020/21. Jana, Uwanja wa Mkapa wakati Simba ikishinda mabao 4-0 dhidi ya Ihefu FC alitupia mabao mawili na kutimiza majukumu yake ndani ya uwanja. Sven amesema:"Sijui haya aneno huwa yanatoka wapi ila ninachojua mimi ni kwamba kila mchezaji ndani ya kikosi cha Simba ni muhimu na wote ninafanya nao mazungumzo. “Wachezaji wangu kwa asilimia kubwa wanapambana na sitaki kuona kwamba wanakuwa wanakosolewa kwa namna yoyote ile. Lawama zao zote lazima zije kwangu na isiwe kwao. "Sina ugomvi na mchezaji na siwezi kumhukumu kwa masuala ya nje ya uwanja mimi ninachohitaji ni kuona kwamba k

DALALI AKOMALIA JINA LAKE KUKATWA, AKIPEWA BARUA KUFANYA MAAMUZI

Image
  MGOMBEA wa nafasi ya uenyekiti ndani ya Simba, Hassan Dalali ambaye jina lake limekatwa, amefunguka kuwa anasubiri akabidhiwe barua ndiyo achukue hatua.   Simba ipo katika mchakato wa kufanya uchaguzi mdogo kuziba nafasi ya mwenyekiti iliyoachwa na Swed Mkwabi.   Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Februari 7,2021.Kamati ya Uchaguzi ya Klabu ya Simba, chini ya mwenyekiti wake, Boniface Lihamwike, imepitisha majina ya wagombea watano kati ya saba waliokuwa wakiwania nafasi hiyo baada ya kufanya usaili Desemba 27 na 28, mwaka huu.   Akizungumza na Spoti Xtra, Dalali alisema amesikia jina lake limekatwa kupitia vyombo vya habari na kuona katika mitandao ya kijamii, lakini bado hajakabidhiwa barua rasmi ya kuelezwa jambo hilo.   "Nimepata habari tu kupitia vyombo vya habari kuwa jina langu limekatwa lakini hadi sasa bado sijakabidhiwa barua, hivyo sitokuwa na nafasi nzuri ya kufanya maamuzi yoyote hadi nitakapopatiwa barua na kujua rasmi kama nimeondolewa.   "Bado ka

KWA FEI TOTO, MKUDE ANAOMBA POO

Image
  KIUNGO Jonas Mkude  wa Simba anaomba poo kwa rekodi kwa Feisal Salum, nyota anayekipiga ndani ya Klabu ya Yanga. Kwa msimu wa 2020/21 Yanga ikiwa imecheza jumla ya mechi 17, Fei ameanza kikosi cha kwanza mechi 15 na kukosekana kwenye mechi mbili huku Mkude ambaye timu yake imecheza jumla ya mechi 15 ameanza kikosi cha kwanza mechi 9. Pia kwa upande wa nidhamu Fei ameonyeshwa kadi moja ya njano licha ya kucheza mechi nyingi akiwa amefunga bao moja kwa Mkude ambaye amecheza mechi chache zaidi ya Fei ameonyeshwa kadi mbili za njano kwenye rekodi zake na hajafunga bao wala kutoa pasi ya bao. Pia Mkude amesimamishwa na Klabu ya Simba kwa kosa la utovu wa nidhamu ambapo anatarajiwa kupelekwa kwenye kamati ya nidhamu ili kujibu tuhuma ambazo zinamkabili kiungo huyo mzawa. Mkude jumla ametumia dakika 814 uwanjani katika mechi 10 ambazo amecheza kwa msimu wa 2020/21 ndani ya Ligi Kuu Bara alimaliza dakika 90 kwenye mechi 9 na mechi moja alitumia dakika 4. Fei amemaliza dakika zote 90 k

KOCHA YANGA AHOFIA REKODI ZA TANZANIA PRISONS

Image
  KOCHA Mkuu wa Yanga, Cedric Kaze, amekiri kuwa mchezo wao wa leo dhidi ya Prisons utakuwa mgumu, hasa kutokana na rekodi nzuri ya wapinzani wao wanapocheza katika uwanja wa nyumbani wa Nelson Mandela uliopo Sumbawanga mkoani Rukwa. Mara ya mwisho timu hizo kukutana ilikuwa katika mchezo wa raundi ya kwanza ndani ya Ligi Kuu Bara msimu huu uliomalizika kwa sare ya bao 1-1.   Kaze ameliambia Spoti Xtra, kuwa ameweka mpango kazi wa kuhakikisha anaufungua ukuta wa Prisons na kupata matokeo mbele yao licha ya wapinzani wake kuwa wagumu.   “Kitu kizuri ni kwamba tumepata muda mzuri wa kujiandaa na mazoezi, na mazoezi ni mazuri na wachezaji wana nia ya kutafuta ushindi kwenye mechi hii na Prisons. “Prisons wana timu nzuri, wanajua kuzuia, wana mwalimu mwenye uzoefu wa ligi lakini na sisi tumejiandaa kulingana na uzito wa mechi, hii.   “Hakuna timu nyingi ambazo zimewafunga wakiwa hapa hivyo tunafahamu tunatakiwa kupandisha pafomansi kwa ajili ya kupata matokeo mazuri,” aliweka nu

KIKOSI CHA YANGA KITAKACHOANZA LEO DHIDI YA TANZANIA PRISONS

Image
 KIKOSI cha Yanga kitakachoanza leo Uwanja wa Neson Mandela dhidi ya Tanzania Prisons kipo namna hii:- Metacha Mnata Kibwana Shomari Yassin Mustapha Lamine Mro Mwamnyeto Bakari Mukoko Tonombe Tuisila Kisinda Feisal Salum Farid Mussa Ntibazonkiza Saido Sarpong Michael Akiba  Faroukh Shikhalo Paul Godfrey Juma Makapu Zawad Mauya Haruna Niyonzima Deus Kaseke Wazir Junior

BOSI WA AZAM FC KUKUTANA NA MWANAFUNZI WAKE WA ZAMANI LEO

Image
  KELVIN Yondani, ingizo jipya ndani ya kikosi cha Polisi Tanzania leo anatarajiwa kuanza kazi dhidi ya bosi wake wa zamani kwenye benchi la ufundi George Lwandamina ambaye anaifundisha Azam FC.   Lwandamina mwenye miaka 57 raia wa Zambia, alimfundisha Yondani alipokuwa kocha wa Yanga msimu wa 2016/18.  Leo anakutana na mwanafunzi wake wa zamani akiwa kwenye maskani mpya ya kucheza huku naye pia akiwa kwenye kibarua kipya cha kufundisha. Yondani amejiunga na Polisi Tanzania kwa dili la mwaka mmoja akiwa ni mchezaji huru baada ya mkataba wake na timu yake ya Yanga kumeguka msimu wa 2019/20 na hakuongeza mkataba mwingine.   Ofisa Habari wa Polisi Tanzania, Frank Lukwaro amesema kuwa taratibu zote kuhusu usajili wa Yondani zimekamilika. “Uongozi umekamilisha kila kitu kuhusu mchezaji wetu Yondani hivyo kwa sasa ni kazi ya benchi la ufundi kuamua kama atamtumia ama la, ila sisi hatuna tatizo naye,” amesema Lukwaro. Huu unakuwa mchezo wa kwanza kwa Azam FC wa mzunguko wa pili

SIMBA YAPIGA HODI CAF KWA SABABU YA MASHABIKI

Image
OFISA Habari wa Simba, Haji Manara amesema kuwa kuelekea mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya FC Platinum kila kitu kipo sawa kwa upande wa maandalizi huku wakiwa wameomba kupewa kibali cha kuongeza idadi ya mashabiki. Mara amesema  Klabu ya Simba, imeliomba Shirikisho la Soka Afrika (Caf) kuwaongezea idadi ya watu kutoka 50% ya mashabiki kuingia uwanjani katika mechi dhidi ya Platinum ya Zimbabwe inayotarajiwa kuchezwa Januari 6, 2021, Uwanja wa Mkapa. Katika mechi dhidi ya Plateau, Caf iliwapa Simba nafasi ya kuingiza mashabiki 50% ya uwezo wa Uwanja wa Mkapa kwa hofu ya ugonjwa wa Covid 19. Manara amesema kuwa wanataka zaidi ya idadi hiyo kutokana na hali ya Tanzania kiusalama wa afya ilivyo jambo ambalo limewafanya watume maombi ya kupewa kibali cha uongezeko la mashabiki zaidi. Pia ameongeza kuwa kutakuwa na punguzo la viingilio ndani ya uwanja ambapo awali ilipangwa kuwa 7,000 ila sasa itakuwa 5,000 mzunguko VIP B na C ilipangwa iwe 20,000 lakini sasa itakuwa 15,00

TANZANIA PRISONS YATAKA KUVUNJA REKODI YA YANGA

Image
  SALUM Kimenya, beki wa Klabu ya Tanzania Prisons amesema kuwa wanahitaji kuvunja rekodi ya Yanga kumaliza mzunguko wa kwanza bila kufungwa kwa kusepa na pointi tatu watakapokutana. Prisons ikiwa imecheza jumla ya mechi 17 imekusanya pointi 21 inakutana na Yanga ambayo imecheza mechi 17 ambazo ni dakika 1,530 bila kupoteza ikiwa na sare nne. Akizungumza na Saleh Jembe, Kimenya amesema kuwa wanatambua kwamba wapinzani wao hawajapoteza hivyo wapo tayari kutibua rekodi hiyo. “Tunajua kwamba hawajapoteza hilo lipo wazi ila nasi pia tunahitaji pointi tatu kwa kuwa nafasi ambayo tupo kwa sasa sio nzuri. "Kikubwa mashabiki wajitokeze kwa wingi kutupa sapoti tupo tayari kwa ajili ya ushindani na tunahitaji kupata matokeo," amesema. Mchezo wa leo unatarajiwa kuchezwa Uwanja wa Nelson Mandela saa 10:00 jioni. Walipokutana Uwanja wa Mkapa, Yanga iligawana pointi mojamoja na Prisons kwa kufungana bao 1-1.

SABABU ZA NYOTA WA YANGA KUIBUKIA GWAMBINA YAWEKWA WAZI

Image
 MABAO 25, ndani ya kikosi cha timu ya Taifa, Taifa Stars ni sababu kubwa ya Klabu ya Gwambina kuvutiwa na mpango wa kumsajili nyota wa zamani wa Klabu ya Yanga, Mrisho Ngasa.   Ngasa anashikilia rekodi ya kufunga mabao mengi zaidi ndani ya kikosi cha Stars kwa wachezaji wa kizazi cha sasa akiwa ameweka kambani mabao 25, akizidiwa mabao matatu tu na mfungaji bora wa muda wote ndani ya kikosi hicho, Sunday Manara ambaye ana mabao 28. Ngassa alikuwa sehemu ya wachezaji 14 walioachwa na Yanga Agosti 3, mwaka huu. Mratibu wa Mashindano wa Gwambina, Mohamed Almas alisema usajili wa nyota huyo ni mapendekezo ya Kocha Mkuu, Fulgence Novatus na Mkurugenzi wa Ufundi, Mwinyi Zahera.   "Suala la usajili wa Ngassa limekamilika kwa kiwango kikubwa, usajili wake ni mapendekezo ya Kocha Novatus ambao umethibitishwa na mkurugenzi wetu wa ufundi, Zahera.   "Kimsingi tunatarajia matokeo makubwa baada ya kukamilisha usajili huu, kwa kuwa Ngassa ni mchezaji mkubwa na hata takwimu zin

ISHU YA KUTOLEWA KWA MKOPO, WATANO SIMBA WAWEKA MGOMO

Image
IMEELEZWA kuwa nyota watano wa Klabu ya Simba ambao wapo kwenye hesabu za kutolewa kwa mkopo wameugomea uongozi kusepa ndani ya kikosi hicho. Wachezaji wanaotajwa kutolewa kwa mkopo ni Kennedy Juma, Miraji Athumani ‘Sheva’, Charles Ilanfya, Ibrahim Ame na Ibrahim Ajibu ambao wamekosa nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza.   Simba imepanga kuwatoa wachezaji hao kwa mkopo baada ya Kocha Mkuu wa timu hiyo, Mbelgiji Sven Vandenbroeck, kupendekeza nyota hao kutolewa ili wakalinde vipaji vyao baada ya kukosa nafasi. Habari zimeeleza kuwa wachezaji hao wamegoma kutolewa kwa mkopo kwa  kuhofia kutelekezwa na timu hiyo. Mtoa taarifa huyo aliwataja baadhi ya wachezaji waliogoma kutolewa kwa mkopo ni Kennedy, Ajibu, Sheva huku Ame akionekana kuwatega viongozi wengine wakipendekeza abakie hapo. Aliongeza kuwa wachezaji waliobakishwa wakiwa katika hatua za mwisho za kutaka kutolewa kwa mkopo ni kiungo Francis Kahata na David Kameta ‘Duchu’ ambao wataendelea kubaki baada ya uongozi k

FT: VPL:SIMBA 4-0 IHEFU

Image
  FT: Simba 4-0 Ihefu Uwanja wa Mkapa Simba inasepa na pointi tatu muhimu na kufikisha pointi 35 Dakika ya 90+2 Mugalu anakosa nafasi ya wazi ndani ya 18 baada ya kumpiga chenga Munish Zinaongezwa dk 3 Dakika ya 90 Teps Evans anaingia anatoka Simchimba Dakika ya 83 Goal Mugalu  Dakika ya 80 Mugalu anaotea inakuwa ni mara ya 7 kwa Simba kuotea Dakika ya 79 Luis anatoka anaingia Dilunga  Dakika ya 71 Ame anapewa huduma ya Kwanza baada ya kuumia ndani ya Uwanja na akatolewa nje nafasi yake ikichukuliwa na Kameta  Dakika ya 64 Luis na Munish wanapewa huduma ya kwanza Dakika ya 63 Luis anakosa nafasi  Dakika ya 60 Chama anaotea Dakika ya 51 Kagere anaotea Dakika ya 49 Mahadhi anatoka anaingia Ngoah, Khamis anatoka anaingia Kinyozi Dakika ya 48 Mahadhi anapewa huduma ya kwanza Dakika ya 47 Manula anaokoa Dakika ya 46 Bwalya anapaisha  Kipindi cha pili KIPINDI cha kwanza  Simba 3-0 Ihefu Uwanja wa Mkapa Mapumziko  Dakika 2 zinaongezwa  Dakika ya 44 Mahundi kadi y

NYOTA GWAMBINA KUMRITHI DUBE NDANI YA AZAM FC

Image
  MTUPIAJI namba moja wa timu ya Gwambina FC, Meshack Abraham mwenye mabao 6 ameingia kwenye rada za Azam FC ambao kwa sasa wanamsaka mbadala wa mshambuliaji wao  Prince Dube. Dube ndani ya Ligi Kuu Bara ndani ya Azam FC inayonolewa na George Lwandamina ametupia jumla ya mabao 6 na ana pasi nne za mabao. Dube kwa sasa yupo kwenye program ya kutibu jeraha lake la mkono alilolipata kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Yanga ambapo Azam FC ilipoteza kwa kufungwa bao 1-0. Tayari ameanza mazoezi mepesi baada ya kutoka nchini Afrika Kusini ambako alikwenda kufanyiwa matibabu zaidi baada ya kuanza kupewa huduma kwenye ardhi ya Bongo, Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Habari zinaeleza kuwa uongozi wa Azam FC umewafuata viongozi wa Gwambina FC ili kuuliza kuhusu kumpata mchezaji huyo. Ofisa Habari wa Azam FC, Zakaria Thabit amesema kuwa wanahitaji kufanya usajili ila itategemea na ripoti ya mwalimu kupitia mapendekezo yake ya wachezaji ambao anawahitaji.

NYOTA HAWA NI MWENDO WA NNENNE NDANI YA LIGI KUU BARA

Image
  LIGI Kuu Tanzania Bara ikiwa inaingia mzunguko wa pili yamefungwa jumla ya mabao 267 huku timu yenye mabao mengi ni Simba. Kinara wa kutupia mpaka muda huu ni John Bocco akiwa amefunga mabao 8 ndani ya Klabu yake ya Simba. Nyota 12 wametupia mabao manne kibindoni ambapo kinara wao ni Lamine Moro wa Yanga ambaye yeye ni namba moja kwa mabeki wa Bongo kwa kucheka na nyavu. Ametupia mabao manne kati ya 28 yaliyofungwa na timu hiyo inayoongoza Ligi Kuu Bara ikiwa na pointi 43. Wengine ni Yacouba Songne mshambuliaji wa kikosi cha Yanga. Michael Sarpong wa Yanga katika mabao hayo manne moja aliwatungua watani zake Simba kwa mkwaju wa penalti, Uwanja wa Mkapa. Deus Kaseke wengi wanapenda kumuita mwaisa kiraka wa Yanga. Bigirimama Blaise ni kinara wa utupiaji ndani ya Namungo na alikuwa ni nyota wa kwanza kutupia msimu wa 2020/21 aliwatungua Coastal Union. Kibu Denis wa Mbeya City ni namba moja kwa kucheka na nyavu kwenye kikosi hicho. Relliants Lusajo wa KMC ni namba moja kwa k

SIMBA KUMBE YAWATISHA WAZIMBABWE KIMTINDO

Image
  ILE kauli mbiu ya Simba kuelekea mchezo wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya FC Platinum ijulikanayo kama War in Dar, kwa kiasi fulani imeonekana kuwatisha Wazimbabwe hao.   Hiyo ni baada ya Kocha Mkuu wa FC Platinum, Norman Mapeza, kuibuka na kusema kwamba mchezo wao marudiano hautokuwa rahisi kutokana kufuatilia rekodi ya Simba katika mechi zake za nyumbani kwenye Ligi Mabingwa Afrika ambazo zinawatisha. Katika mchezo wa kwanza uliochezwa Jumatano iliyopita ijini Harare, Zimbabwe, FC Platinum iliibuka na ushindi wa bao 1-0.   Timu hizo zinatarajiwa kurudiana Januari 6, mwakani ambapo mshindi wa jumla anafuzu hatua ya makundi, huku atakayepoteza akiangukia hatua ya mtoano ya Kombe la Shirikisho Afrika.   Akizungumza na Spoti Xtra, Mepeza alisema: “Ukweli uliowazi ni kwamba, wamekuwa na rekodi nzuri katika uwanja wao wa nyumbani, hilo jambo kiasi fulani linatia hofu lakini bado haiwezi kutukwamisha kusimamia mipango yetu, tumeshinda nyumbani lakini hata nje ya

WAWILI NAMUNGO KUIKOSA COASTAL UNION KESHO

Image
 NAMUNGO FC inayonolewa na Kocha Mkuu, Hemed Morroco kesho Desemba 31 itakuwa na kazi ya kusaka pointi tatu mbele ya Coastal Union. Mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Majaliwa,Namungo iliibuka na ushindi wa bao 1-0 lilipachikwa na kinara wa mabao ndani ya kikosi hicho, Bigirimana Blaise. Akizungumza na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa Namungo FC, Kidamba Namlia amesema kuwa wachezaji wapo tayari na kila kitu kinakwenda sawa wanasubiri wakati ufike. "Tupo sawa na kila kitu kinakwenda sawa, kuna baadhi ya wachezaji ambao tutawakosa ndani ya kikosi ikiwa ni pamoja na beki Kristom na mshambuliaji Adam Salamba. "Krmstom yeye ni mgonjwa na Salamba yeye bado hajarejea kwenye ubora wake hivyo wapo Dar wakiendelea na matibabu," amesema.

ARTETA AGOMA KUBADILI MPANGO WAKE KWENYE USAJILI

Image
  MIKEL Arteta, Kocha Mkuu wa Arsenal amesema kuwa ushindi wa mechi mbili mfululizo ndani ya Ligi Kuu England hautabadilisha mpango wa yeye kuhitaji kuboresha kikosi chake. Arteta ameongoza kikosi hicho kushinda mara mbili baada ya mchezo wake uliopita kushinda mabao 3-1 dhidi ya Chelsea na usiku wa kuamkia leo kushinda bao 1-0 dhidi ya Brighton. Bao pekee la ushindi lilipachikwa na Alexandre Lacazette dakika ya 66 na kuifanya Arsenal kusepa mazima na pointi tatu Uwanja wa Falmer. Arteta amesema:-"Matokeo ambayo tunayapata ndani ya ligi hayatabadilisha mpango wangu kwenye suala la usajili hivyo lazima mipango ikamilike. "Tupo kwenye wakati mgumu kwa sasa ambao tunapitia na ratiba yetu ni ngumu, hivyo kushinda mara mbili haiwezi kubadili mpango wangu kuelekea kwenye dirisha la usajili" .

MBELGIJI SIMBA AKWAA KIZINGITI CHA KUFUNGIA MWAKA

Image
  MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Bara, Simba leo wanakutana na ngoma nzito ya kufungia mwaka 2020 kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara utakaochezwa Uwanja wa Mkapa ambao ni Ihefu FC. Ikiwa kwenye presha ya kupunguza pointi inazodaiwa na watani zao wa jadi Yanga inakutana na Ihefu ambayo inapambania nafasi ya kubaki ndani ya Ligi Kuu Bara kwa kuwa ipo nafasi ya 16 na pointi zake 13 baada ya kucheza mechi 17. Simba ipo nafasi ya pili na pointi 32 baada ya kucheza mechi 14 imeachwa kwa jumla ya pointi 11 na watani zao wa jadi Yanga ambao wana pointi 43 baada ya kucheza mechi 17. Sven anakutana na ngoma nzito kwa kuwa anakutana na benchi la ufundi la Ihefu linaloongozwa na Zuber Katwila ambaye alimbania pointi tatu Uwanja wa Jamhuri wakati ule akiifundisha Mtibwa Sugar kwenye sare ya kufungana bao 1-1. Kizingiti kingine anachokutana nacho ni kipa namba moja wa Ihefu ambaye ni Deogratius Munish, ‘Dida’ amekaa ndani ya Simba kwa muda wa msimu mmoja, 2018/19 hivyo anajua mbinu za wapinzani wak

HAJI MANARA AFUNGUKIA HATMA YAKE YA KUSEPA SIMBA

Image
 OFISA Habari wa Simba , Haji Manara amesema kuwa bado atabaki kuwa ndani ya Simba kuendelea na majukumu yake licha ya habari kueleza kuwa amesimamishwa na mabosi zake. Hivi karibuni ilikuwa ikielezwa kwamba Manara amesimamishwa ndani ya Simba jambo ambalo limemfanya asizungumze masuala ya timu hiyo jambo ambao alilikanusha kwa kusema kwamba alipewa mapumziko na uongozi baada ya kufunga ndoa. Kupitia ukurasa wake wa Intagram, Manara amesema:-"Huu ukubwa wa jina langu unaniponza, u maarufu wangu unawaumiza wengine. "Sikuwahi kutaka kuwa hivi, lakini kazi yangu naamini imewavutia wengi na Mungu akaamua kunipandisha. "Please Please Please (Tafadhali) Wanasimba mimi Haji wenu bado nipo nanyi na nitaendelea kuwa msemaji wenu hadi pale riziki yangu itakapokwisha, ( Hatatokea mmoja wetu kubaki milele iwe kwa kifo au vinginevyo ) Waambieni wenye kuandika tetesi za kuondoka kwangu, mimi mtu dhaifu lakini ni mjuzi mno katika mambo ya mawasiliano ya umma na nina uzoefu mk

MTIBWA SUGAR YATUMA UJUMBE KWA RUVU SHOOTING

Image
 UONGOZI wa Mtibwa Sugar umesema kuwa upo tayari kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Ruvu Shooting ambao utakuwa ni wa zmunguko wa pili. Mchezo wa kwanza kwa msimu wa 2020/21 timu hizi zilitoshana nguvu ya bila kufungana na waligawana pointi mojamoja. Ofisa Habari wa Mtibwa Sugar,Thobias Kifaru amesema wapo tayari kwa ajili ya mchezo huo ambao utakuwa na ushindani mkubwa. "Tuna mchezo mgumu na wenye ushindani mkubwa ila sisi tupo tayari na tunahitaji kupata pointi tatu muhimu ndani ya uwanja. "Mchezo wetu wa kwanza tulitoshana nao nguvu na inatufanya tuzidi kujipanga kwa ajili ya mchezo wetu ujao, mashabiki wajitokeze kwa wingi kutupa sapoti," amesema. Utakuwa ni mchezo wa kwanza ndani ya 2021 kwa timu hizi mbili kukutana ndani ya uwanja. Utachezwa Januari 2,2021.

SABABU ZA MKUDE KUCHIMBISHWA SIMBA ZATAJWA

Image
 IMEELEZWA kuwa sababu ya nyota wa kikosi cha Simba, Jonas Mkude kusimamishwa na mabosi wa timu hiyo ni mfululizo wa makosa ya mara kwa mara ikiwa ni pamoja na unywaji pombe kupitiliza. Kiungo huyo mkabaji Desemba 28 amesimamishwa na Simba huku akitarajiwa kupelekwa kamati ya nidhamu kujibu shutuma zinazomkabili. Ndani ya Ligi Kuu Bara chini ya Kocha Mkuu, Sven Vandenbroeck kikosi hicho kikiwa kimecheza jumla ya mechi 14 yeye amecheza mechi 10 akikosekana kwenye mechi nne. Katika mechi hizo 10 alizocheza moja alianzia benchi huku tisa akianza kikosi cha kwanza ndani ya timu hiyo inayopambana kutetea taji la ligi Habari zinaeleza kuwa nyota huyo alikunywa kupita kiasi kabla ya timu yake kuvaana na FC Platinum ya Zimbabwe wakati Simba ikipoteza kwa kufungwa bao 1-0. "Mkude amekuwa na tabia za kunywa kupita kiasi hata kabla ya mechi ngumu na muhimu, licha ya kuonywa amekuwa akirudia kufanya makosa hayo hata nchini Nigeria alifanya hivyo hata Zimbabwe. "Pia amekuwa ni mwe

MICHAEL SARPONG WA YANGA APOTEZWA NA KARIHE WA DODOMA JIJI

Image
  SEIF Karihe, nyota wa kikosi cha Dodoma Jiji aliyemtungua Metacha Mnata kipa namba moja kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha amempoteza mshambuliaji wa Yanga, Michael Sarpong kwa idadi ya mabao. Karihe alimtungua Mnata kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara wakati Yanga ikishinda kwa mabao 3-1 na kusepa na pointi tatu jumlajumla. Karihe ametupia jumla ya mabao matano ndani ya ligi akimzidi bao moja nyota huyo Sarpong mwili jumba mwenye mabao manne ndani ya ligi. Karihe ametupia mabao matano huku katika mabao hayo matano hajafunga bao hata moja kwa penalti ilikuwa ni jitihada zake binafsi za kusaka ushindi kwa timu yake. Sarpong ametupia bao moja kwa mkwaju wa penalti ilikuwa Uwanja wa Mkapa, wakati Yanga ikitoshana nguvu ya kufungana bao 1-1 na Simba.

ORODHA YA WACHEZAJI WATANO WA SIMBA WALIOITWA STARS

Image
  NYOTA watano wa kikosi cha kwanza cha Simba wameitwa ndani ya kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania kinachonolewa na Kocha Mkuu, Ettiene Ndayiragije. Nyota hao ni kipa namba moja Aish Manula, beki wa kulia Shomari Kapombe beki kiraka Erasto Nyoni naye jina lake limejumuishwa kikosini. Wengine wawili ni kiungo Said Ndemla mwenye sifa ya kupiga mashuti yenye uzito akiwa nje ya 18 na mshambuliaji bora wa muda wote ndani ya Bongo, John Bocco mwenye zaidi ya mabao 100.  Kikosi cha Stars kinatarajiwa kuingia kambini Januari Mosi kwa ajili ya maandalizi ya Chan 2021 ambapo kitacheza mechi mbili za kirafiki za kimataifa na timu ya Congo.