Posts

Showing posts from August, 2021

VIDEO:MABILIONI YA YANGA KUTEKA JIJI, VITA YA MORRISON NA MANARA YAENDELEA

Image
MABILIONI ya Yanga kuteka ligi, vita ya Bernard Morrison na Haji Manara yaendelea.  

AZAM FC WAMPA DILI LA MWAKA MMOJA BEKI MCAMEROON

Image
KIKOSI cha Azam FC kilifunga dirisha la usajili kwa ajili ya msimu wa 2021/22 katika Ligi Kuu Bara pamoja na Kombe la Shirikiho na mashindano mengine ambayo watashiriki.  Ni usajili wa beki wa kati raia wa Cameroon, Yvan Lionnel Mballa alifunga usajili kwa timu hiyo ambayo imeweka kambi nchini Zambia. Ni dili la mwaka mmoja kasaini beki huyo akitokea Klabu ya Forest Rangers ya Zambia. Mballa amefunga zoezi la usajili kwenye dirisha lililofungwa usiku wa Agosti 31.

VIDEO:SIMBA: BEKI MPYA WA SIMBA HATARI, ANATUMIA MIGUU YOTE

Image
UONGOZI wa Simba umebainisha kuwa usajili ambao wamefanya ni mzuri kwa kuzingatia umri pamoja na uwezo wa wachezaji huku ukibainisha kuwa ujio wa beki Henock Inonga kutoka Congo ni moja ya sajili bora kwao. Pia ana uwezo wa kutumia miguu yote miwili na beki wa kiwango cha juu, hakuna mfano wake ni kwa mujibu wa Crestius Magori aliyekuwa CEO wa timu hiyo ila kwa sasa CEO ni Madam Barbara Gonzalez.  

YANGA KAZI INAENDELEA KWA AJILI YA MSIMU MPYA WA 2021/22

Image
 MABINGWA wa taji la Kuu Bara mara 27 ndani ya ardhi ya Tanzania Yanga wameendelea kujiweka sawa kwa ajili ya msimu wa 2021/22 licha ya baadhi ya nyota wa timu hiyo kuwa katika majukumu katika timu zao za taifa. Mataifa mengi ya Afrika kwa sasa ni maandalizi kuelekea katika mechi za kufuzu Kombe la Dunia jambo ambalo limefanya idadi ya wachezaji katika timu kupungua. Miongoni mwa wachezaji wa Yanga walioitwa katika timu zao za taifa ni pamoja na Khalid Aucho, raia wa Uganda pia yupo Ramadhani Kabwili, Feisal Salum na Dickson Job hawa ni wazawa. Ambao wameendelea na mazoezi miongoni mwao ni pamoja na Dickson Ambundo ambaye, Deus Kaseke, Paul Godfrey wengi hupenda kumuita Boxer. Kwa msimu wa 2020/21, Yanga ilimaliza ikiwa nafasi ya pili baada ya kukusanya pointi 74 na ilipachika mabao 52 katika mechi 34. Iliweka kambi kwa muda mfupi nchini Morocco kisha ghafla ikarejea ndani ya ardhi ya Tanzania na kwa sasa imeweka kambi Avic Town, Kigamboni.

MFAUME MFAUME AZIGOMEA KEJELI ZA MWAKINYO

Image
 BONDIA wa ngumi za kulipwa nchini Mfume Mfaume amepinga vikali kauli ya Hassan Mwakinyo ya kujiita yeye ni Professional Boxer na wengine kuwa mabondia wakawaida jambo ambalo halina ukweli wowote ikiwa wote wanacheza ngumi za kulipwa. Mfaume ametoa kauli hiyo kufuatia kauli iliyotolewa na Mwakinyo baada kuulizwa juu ya kupigana na Twaha Kiduku ambapo alijibu kwa sasa yeye anafanya Proffesional Boxing tofauti na bondia Twaha Kiduku pamoja na mabondia wengine. Mfaume amesema:- “Mabondia wanaocheza ngumi za kulipwa nchini wote ni kama watoto wa mama mmoja hivyo wote ni Professional Boxers haijalishi bondia huyo amecheza sana na mabondia kutoka nje ya nchi au ndani ilimradi bondia huyo awe ametoka kwenye ngumi za ridhaa na kuingia kwenye ngumi za kulipwa. “Lakini ninanatarajia pia kupanda ulingoni Octoba 30, mwaka huu na pambano hilo ambalo limeandaliwa na Kepteni Seleman Semunyu, nimeanza maandalizi nikiwa kama bondia wa kulipwa,” alisema Mfaume.

USAJILI ULAYA, MAJEMBE HAYA YALILETA MSHTUKO

Image
  USAJILI wa Ulaya kwa ajili ya maandalizi ya msimu wa 2021/22 unatajwa kuwa na maajabu kibao kutokana na kutokea mambo ambayo wengi hawakutarajia ikiwa ni pamoja na kusepa kwa Lionel Messi kutoka Barcelona mpaka PSG, Cristiano Ronaldo kutoka Juventus na kurejea Manchester United pamoja na Romelu Lukaku kutoka Inter Milan na kurejea Chelsea. Mabadiliko hayo pia yanatajwa kuchangiwa na kushuka kwa uchumi kwa timu nyingi duniani pamoja na sheria ambazo zimewekwa katika masuala ya usajili na suala kubwa lililosababisha kuporomoka kwa uchumi ni janga la Corona. Ilikuwa ngumu kwa wengi kufikiria kwamba Messi angesepa Barcelona kwa kuwa alikuwa tayari kusaini dili la miaka mitano ili abaki ndani ya Uwanja wa Camp Nou na alikuwa tayari kupunguziwa mshahara raia huyo wa Argentina ila mambo yakabuma. Vilevile Ronaldo yeye dili lake ndani ya Juventus lilikuwa limebakisha miezi 12 kukamilisha miaka minne kwa kuwa alisaini hapo 2018 akitokea Real Madrid lakini msimu uliopita mambo yalikuwa

MICHAEL SARPONG KULIPWA MKWANJA MREFU KWA MWEZI

Image
  WAKATI Yanga ikitambulisha wachezaji wapya kwa ajili ya msimu ujao, mshambuliaji wa timu hiyo, Mghana,Michael Sarpong   amejiunga na Klabu ya Al Nahda ya Saudi Arabia kwa mkataba wa miaka miwili huku akikomba mshahara wa dola 12,000 sawa Sh milioni 27 kwa mwezi.   Sarpong alijiunga na Yanga msimu uliopita kwa mkataba wa miaka miwili akitokea Rayon Sport ya Rwanda lakini alishindwa kuisaidia Yanga kwenye eneo la ushambuliaji hali iliyopelekea kuvunjwa kwa mkataba wake wa mwaka mmoja uliobakia.    Meneja wa mshambuliaji huyo, Mnyarwanda, Alex Kamanzi alisema kuwa tayari mchezaji wake ameshajiunga na Al Nahda baada ya kumalizana na Yanga kufuatia kufikia makubaliano ya kuvunja mkataba wake.   “Sarpong ameshapata timu yupo Saudia Arabia amejiunga na Al Nahda kwa mkataba wa miaka miwili baada ya kuachana na Yanga kufuatia kufikia makubaliano ya kuvunja mkataba wake.   “Kitu kikubwa cha kushukuru upande wetu wa kuhakikisha tumepata sehemu ya mchezaji wetu kucheza kwa sababu ndiyo

HAYA HAPA MAAGIZO YA MO KWA KOCHA DIDIER GOMES

Image
  MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi wa Simba, Mohammed Dewji ‘MO’ amempa maagizo mazito kocha mkuu wa klabu hiyo Mfaransa, Didier Gomes kuhakikisha klabu hiyo inatwaa makombe yote ya ndani ambayo watashiriki na kufika angalau nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.   Msafara wa mwisho wa Simba uliokuwa nchini Morocco kwa ajili ya maandalizi ya kabla msimu ulirejea rasmi Jumapili, baada ya kipindi cha wiki tatu za maandalizi.   Katika kipindi hiko cha wiki tatu Simba walicheza michezo miwili ya kirafiki dhidi ya FAR Rabat na Olympique Club de Khouribga ambapo michezo yote iliisha kwa sare.   Kaimu Ofisa Habari wa Klabu ya Simba, Ezekiel Kamwaga alisema: “Baada ya kumaliza kambi yetu ya kwanza ya maandalizi ya kabla ya msimu ‘preseason’ kule Morocco na kikosi kurejea hapa nchini, sasa tunajipanga kuwa na kambi ya pili ya nje ya nchi ambayo tutaiweka wazi.   “Nikuhakikishie kuwa tumejizatiti kuhakikisha tunapiga hatua moja zaidi msimu ujao kulinganisha na msimu uliopita katika

SAUTI: MAKAMBO AAHIDI MAKUBWA YANGA,KUWAJAZA KAMA KAWAIDA

Image
MSHAMBULIAJI wa Yanga, Heritier Makambo amewaahidi mashabiki wa Yanga makubwa kutokana na kurejea Bongo kwa mara nyingine tena.  

KAGERASUGAR YAIKAMUA SIMBA MILIONI 40, KISA MHILU

Image
RASMI sasa Yusuph Mhilu ni mali ya Simba baada ya uhamisho wake kukamilika na mabosi wa Simba kuweka mkwanja mezani kwa ajili ya kuvunja mkataba wake. Taarifa rasmi kutoka Kagera Sugar imeeleza namna hii:" Tumefikia makubaliano ya pande zote mbili (Kagera Sugar FC na Simba SC) juu ya uhamisho wa aliyekuwa mchezaji wetu Nyota Yusuph Valentine Mhilu kwa Dau la Tsh.40M. "Yusuph Mhilu alisaini kandarasi ya miaka miwili kuitumikia Kagera Sugar Football Club mwaka jana 2020. Hivyo uhamisho huu wa Yusuph Mhilu kwenda Simba ni Uhamisho ambao umehusisha kuvunja mkataba wake wa mwaka mmoja uliosalia ndani ya Klabu ya Kagera Sugar. "Tunamtakia kila la kheri huko aendako na Mungu amsimamie katika kukiendeleza kipaji chake,". Usajili wa Mhilu kuibukia Simba ulikuwa ni wa ghafla baada ya viongozi wa Simba kumdaka mazimamazima Dar alipotoka na timu ya taifa ya Tanzania kwa vijana chini ya umri wa miaka 23 kushiriki Cecafa. Alisaini dili la miaka mitatu jambo ambalo lili

EXCLUSIVE:JESHI KAMILI LA RUVU SHOOTING 2021/22, MASAU APIGA MKWARA

Image
IKIWA leo Agosti 31 dirisha la usajili linatarajiwa kufungwa ifikapo saa sita kamili usiku, Ruvu Shooting wamekamilisha usajili kwa kuwatangaza nyota wao wapya na wale waliokuwa ndani ya kikosi hicho kwa msimu wa 2020/21. Pia imepandisha nyota wengine kutoka kikosi cha vijana.  

SENZO AWA C.E.O YANGA

Image
  MAKAMU Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga, Fredrick Mwakalebela leo Agosti 31, 2021 amemtangaza, Senzo Mbatha kuwa Kaimu Mtendaji Mkuu (C.E.O) wa Klabu hiyo. Kwa majukumu hayo ana jukumu la kusimamia mchakato wa mabadiliko kufikia mwisho na aliyekuwa Kaimu Katibu Mkuu wa Klabu hiyo, Hajji Mfikirwa atakuwa Mkurugenzi wa Fedha na Utawala. Fredrick Mwakalebela ametangaza hayo baada ya Katiba ya Yanga kubadilishwa baada ya wanachama wa Klabu hiyo kupitisha mchakato wa mabadiliko kwa asimia mia. Mbata awali alikuwa mshauri mkuu wa Yanga kuelekea kwenye mabadiliko baada ya kubwaga manyanga ndani ya Simba ambapo alikuwa kwenye nafasi hiyo. Ndani ya Yanga anakuwa ni Mtendaji Mkuu wa mpito, (Interm CEO) wa Klabu ya Yanga kufuatia utekelezwaji wa mfumo wa uendeshaji wa klabu.

PANAPOVUJA YANGA PAMEONEKANA, MUDA WA KUIFANYIA KAZI

Image
 AGOSTI 15, 2021 kikosi cha Yanga kiliondoka hapa nchini kuelekea Afrika Kaskazini, kwenye nchi ya Morocco kwa ajili ya kuweka kambi iliyotarajiwa kutumia siku kumi kwa ajili ya maandalizi ya kabla ya msimu ‘Pre season’, ambapo baada ya safari ya siku mbili walitua Jijini Marrakech Agosti 17, ambapo walianza rasmi mazoezi. Kambi hiyo ilihusisha wachezaji wote wa Yanga ambao watatumika msimu ujao wakiwemo nyota wapya kumi ambao wamesajiliwa kwenye dirisha kubwa la usajili ambalo litafungwa rasmi Agosti 31, mwaka huu. Leo ifikapo saa sita usiku, dirisha la usajili litafungwa kwa mujibu wa taarifa kutoka Shirikisho la Soka Tanzania, (TFF). Baada ya siku sita za programu ya mazoezi hayo ambayo yalikuwa yakiwasilishwa kwa wapenzi na wadau wa Yanga kupitia mitandao ya kijamii ya klabu hiyo, ghafla kambi hiyo ilivunjwa. Taarifa rasmi kutoka kwenye Uongozi wa Yanga zilieleza kuwa kutokana na sababu mbalimbali na kwa maslahi mapana ya klabu hiyo uongozi uliamua kusitisha kambi hiyo na kue

NYOTA HAWA 12 WAPIGWA CHINI COASTAL UNION, MBISSA ATAMBULISHWA

Image
  WAKATI wakimtambulisha Mussa Mbissa kuwa kipa wao ndani ya kikosi cha Coastal Union ya Tanga itakayokuwa chini ya Kocha Mkuu, Melis Medo wote wakiwa wamesaini madili ya miaka miwili nyota 12 wamepigwa chini mazima. Taarifa rasmi iliyotolewa na Coastal Union imewataja nyota hao kuwa ni:- Adil Nasor Ayoub Masoud Mudhathir Abdalah Hassan Kibailo Salum Ally Salum Peter Mwangosi Seif Bihaki Hussein Abel Muhidin Mbuki Nelson Haule Christopher Edward Issa Yusuph

SIMULIZI YA ALIYESAIDIWA BAADA YA KULAGHAIWA, POLISI WALIPEWA RIPOTI

Image
SIMULIZI ya jirani aliyesaidiwa baada ya kufanyiwa ulaghai, alitoa ripoti Polisi. Suala la ulaghai ni suala ambalo limekithiri mizizi kwenye ulimwengu wa sasa haswa nchini  Kenya. Siku haiwezi kamilika kabla mtu moja ama wawili kulia kutokana na ulaghai wa pesa ama  kitu kingine cha dhamana. Mtu anapolaghaiwa huwaacha akiwa amesononeka ajabu na hata wakati  mwingine anaweza kukumbwa na mzongo wa mawazo ama hata mshtuko wa moyo kwani hutegemea  ni nini ambacho amelaghaiwa kwa wakati wowote ule.  Tuliishi katika mji wa Eldoret ambapo  mume wangu alikuwa mfanyibiashara wa kuuza bidha za ujenzi. Tuliifanya kazi ile na yeye kwani  ilikuwa kazi ambayo tuliitegemea na ama kwa hakika ilileta mapato mengi zaidi.  Jirani yetu Kamau  pamoja na marafiki wake walikuja nyumbani siku moja huku wakiwa na ajenda kwamba walikuwa  wakijua mahali ambapo tungepata bidhaa za ujenzi za kuuza na ambazo zilikua bei rahisi. Mimi na mume wangu hatukusita kwani tulipokea suala lile kwa mikono yote kwani  in

RONALDO NI AREJEA MANCHESTER UNITED

Image
  SASA ni rasmi Cristiano Ronaldo raia wa Ureno msimu wa 2021/22 ni mali ya Manchester United baada ya mabosi wa timu hiyo kumtambulisha rasmi kwa kusema kwamba yupo nyumbani. Taarifa rasmi iliyotolewa katika Ukurasa wa Instagram wa Manchester United uliandika maneno mafupi kwamba Cristiano yupo nyumbani na kusindika na picha ya Cristiano Ronaldo katika mapozi tofauti. Gumzo kubwa katika usajili wa Ulaya awali lilikuwa kwa Harry Kane wa Tottenham pamoja na Jack Grealish aliyekuwa anakipiga ndani ya Aston Villa ila kwa sasa ni mali ya City kabla ya United kutibua dili la Ronaldo kujiunga na City akitokea Klabu ya Juventus.  Ni dili la miaka miwili amesaini Ronaldo ndani ya Manchester United ambapo anarudi hapo baada ya miaka 12 kupita na alipokuwa hapo alifunga jumla ya mabao 118 katika mechi 292 alizocheza kati ya mwaka 2003 na 2009 alitwaa mataji matatu ya Ligi Kuu England,  Ligi ya Mabingwa Ulaya na FA Cup pia alitwaa mataji mawili ya League Cup. Anakwenda kuwa chini ya Kocha

DIRISHA LINAFUNGWA, KWA WALE AMBAO MAMBO BADO WAKAMILISHE

Image
 NI masaa tu kwa sasa yamebaki kabla ya dirisha la usajili kwa msimu wa 2021/22 kufungwa. Leo Agosti 31 milango iliyokuwa wazi inafungwa. Sarakasi zimekuwa zikionekana kwenye timu zote kuhusu usajili hilo ni sawa. Ipo hivyo duniani kote hasa pale ambapo usajili unapofunguliwa ni asili ya mpira na mara nyingine bila hayo ule umakini unapungua kidogo. Haina maana kwamba haya makosa yanapaswa kuwepo hapana ni mbaya kujirudia mara kwa mara kwa kuwa itafika wakati kunakuwa na muda mwingi wa kusikiliza kesi kuliko kufanya maendeleo kwa ajili ya timu zetu kusaka mafanikio. Kwa namna soka letu la Bongo lilivyo nina amini kwamba zipo timu ambazo mpaka sasa hazijakamilisha usajili. Unaweza ukashangaa lakini huu ni ukweli na ipo wazi kabisa zipo timu wakati huu zinaanza kuingia sokoni kusaka wachezaji. Viongozi wengine kwa sasa wanaanza kuwavutia waya wachezaji wao ili kujua kuhusu hatma yao kwa kuboresha mikataba yao. Kawaida na watakaoanza kumalizia leo nadhani watajipongeza kwamba wa

MAKAMBO APIGA HESABU ZA KUFUNGA MABAO MENGI YANGA

Image
  MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Yanga raia wa DR Congo, Heritier Makambo ameweka wazi kuwa malengo yake makubwa msimu ujao ni kuhakikisha anafunga mabao mengi zaidi ya 17 aliyofunga kwenye msimu wake wa mwisho alipokuwa Yanga wa 2018/19.   Makambo amerejea Yanga akitokea klabu ya Horoya AC ya Guinea, ambapo hii itakuwa mara ya pili kwake kuwatumikia Wananchi, akiwahi kuichezea klabu hiyo kwa mafanikio kwa kipindi cha msimu mmoja wa 2018/19.   Katika msimu huo, Makambo alifanikiwa kufunga mabao 21 kwenye michezo 40 ya michuano yote, ambapo kwenye Ligi Kuu Bara pekee alifunga mabao 17.   Akizungumza na  Championi  Jumatatu,  Makambo alisema: “Najua kuna matarajio makubwa sana ya mashabiki wa Yanga juu ya kikosi chao kwa msimu ujao hasa kutokana na usajili ambao umefanyika, hususani kwa mchezaji kama mimi ambaye tayari wengi wamepata nafasi ya kuniona.   “Hivyo najua nina deni kubwa la kuhakikisha ninafunga mabao, kwa sasa siwezi kusema nitafunga mabao mangapi lakini, nataka kufu

VIDEO: YANGA YAWATANGAZIA VITA WANAIJERIA,BANDA AIBUA JAMBO SIMBA

Image
YANGA yawatangazia vita Wanaijeria,Banda aibua jambo Simba  

TROY DEENEY MALI YA BIRMIGHAM

Image
KLABU ya Birmigham imethibitisha kukamilisha usajili wa Troy Deeney kwa dili la miaka miwili baada ya mshambuliaji huyo kuyeyusha jumla ya miaka 11 akiwa ndani ya Watford inayoshiriki Ligi Kuu England. Deeney mwenye miaka 33 amesema kuwa kwa kila jambo ambalo alifanya ndani ya timu hiyo kwake ni furaha hivyo anahitaji kuweza kupata changamoto mpya katika maisha mapya ambayo anakwenda kuayaanza. Anakwenda kujiunga na timu yake ya utotoni Birmingham inayoshiriki Championship baada ya kukubali dili lake la miaka miwili ambalo litameguka mwaka 2023 ukiwa na kipengele cha kumuongezea dili lingine tena ikiwa ataweza kufanya vizuri. Mshambuliaji huyo alijiunga na Klabu ya Watford mwaka 2010 akitokea Klabu ya Walsall na aliweza kufunga jumla ya mabao 140 huku lile lililopata umaarudfu ni lile alilowatungua Leicester City 2013 na mabao hayo alifunga kwenye mechi 419 ambazo alicheza.

LIVERPOOL WATAJWA KUWA KWENYE RADA ZA MASTAA KIBAO, TRAORE,MBAPPE

Image
WAKATI dirisha la usajili Ulaya likitarajiwa kufungwa leo Agosti 31 usiku, Liverpool inatajwa kuwa katika hesabu za kuwa kwenye anga za za kunasa saini za baadhi ya nyota. Miongoni mwa wanaotajwa kuwa katika rada hizo ni Saul Niguez ambaye ni kiungo ndani ya Klabu ya Atletico Madrid na timu ya taifa ya Hispania ana umri wa miaka 26 alikuwa anatajwa kuwaniwa pia na Manchester United. Yupo pia Renato Sanches kiungo anayecheza ndani ya Ligue 1 akiwa katika Klabu ya Lille na ana umri wa miaka 24 alikuwa anatajwa pia kuwaniwa na Wolves. Kylian Mbappe mshambuliaji wa PSG huyu Real Madrid wanampigia hesabu kali wanashindana katika dau tu kwa sasa na Adama Traore, mwenye miaka 25 akiwa anacheza winga ndani ya Wolves alikuwa anatajwa kuibukia ndani ya Spurs pia.

KIUNGO WA AZAM KUIBUKIA KENYA

Image
  KIUNGO wa kimataifa wa Kenya na Klabu ya Azam, Kenneth Muguna leo ameondoka kwenye kambi ya Azam FC iliyopo Zambia kwa ajili ya kujiunga na timu ya taifa ya Kenya.   Azam ipo Ndola, Zambia kwa ajili ya maandalizi ya kabla ya msimu ya takribani wiki moja na nusu, ambapo wakiwa huko wamepanga kucheza michezo minne ya kirafiki kabla ya kurejea Tanzania Septemba 5, mwaka huu.   Watakaporejea Azam watakuwa kwenye maandalizi ya mwisho ya mchezo wao wa kwanza wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Horseed ya Somalia, unaotarajiwa kuchezwa kati ya Septemba 10 hadi 12, mwaka huu.   Akizungumza na Championi Jumatatu, Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Azam, Zakaria Thabith ‘Zaka Zakazi’ alisema: “Kikosi chetu kinaendelea vizuri na maandalizi ya kabla ya msimu ‘Preseason’ hapa Ndola Zambia.   “Tunatarajia kuwa kiungo wetu wa kimataifa wa Kenya Kenneth Muguna ataondoka kambini kwa ajili ya kujiunga na timu ya taifa ya nchi yao.” Mchezo wa pili Azam FC ilicheza na Kabwe War

MUGALU ATAJWA NA BEKI MPYA WA SIMBA BAKA

Image
  BEKI mpya wa Simba, Henock Inonga Baka amesema kuwa Chris Mugalu ndiye mchezaji ambaye anampa ushirikiano mkubwa katika kuyazoea kwa haraka maisha yake ndani ya Simba.   Baka ambaye ni beki wa Kati, amesajiliwa na Simba akitokea katika Klabu ya DC Motema Pembe ya nchini DR Congo.     Baka amesema kuwa Mugalu amekuwa akimpa ushirikiano mkubwa wa kuhakikisha kuwa anayazoea mazingira mapya ndani ya Simba pamoja na kumfundisha jinsi ya kuongea Kiswahili.   “Mimi na Mugalu ni marafiki tangia zamani, nimefurahi kumkuta hapa ndani ya Simba yeye ndiye anafundisha kila kitu kuhusu Simba na kuzungumza kiswahili hivyo nashukuru kwa hilo,". Nyota huyo anatarajiwa kuwa katika maisha mapya ndani ya ardhi ya Tanzania kwa msimu mpya wa 2021/22 akiungana na nyota wengine kama Israel Mwenda pamoja Peter Banda ambao wamesajiliwa na timu hiyo. Kazi kubwa ni kuweza kutetea mataji ambayo ilitwaa kwa msimu uliopita wa 2020/21 pamoja na kuweza kuweka rekodi ya kutinga hatua ya robo fainali

CRISTIANO RONALDO AKAMILISHA MASUALA YA VIPIMO KWA AJILI YA KUJIUNGA NA UNITED

Image
CRISTIANO Ronaldo, tayari ameshakamilisha masuala ya vipimo hivyo yupo tayari kurejea kwenye timu yake ya zamani ya Manchester United na kinachosubiriwa kwa sasa ni utambulisho wake pekee. United wameeleza kuwa wamefikia makubaliano mazuri na Juventus ambapo alikuwa anacheza mshambuliaji huyo mwenye miaka 36 kwa ajili ya kuipata saini yake. Masuala binafsi kati ya mchezaji na timu yameshapitishwa na amekubali kusaini dili la miaka miwili kwa sasa dili lake lipo kwenye hatua za mwisho kabla ya dirisha la usajili kufungwa usiku wa leo Jumanne ya Agosti 31. Nyota huyo anakwenda kurejea kwenye Ligi Kuu England anatajwa kuwekewa mkwanja mrefu na atakuwa anapokea pia mshahara mnono kwa wiki jambo ambalo lilimfanya akubali kurejea hapo. Ronaldo alifunga jumla ya mabao 118 alipokuwa ndani ya Manchester United katika mechi 292 ambazo alicheza kati ya mwaka 2003 na 2009.

VIDEO: MZARAMO AMLIPUA HAJI MANARA

Image
MZARAMO, shabiki wa Simba amlipua Haji Manara ambaye alikuwa ni Ofisa Habari wa Simba ila kwa sasa ni mali ya Yanga baada ya kutambulishwa rasmi Agosti 24.  

MJUMBE HAZARD MAFANIKIO KAYAACHA CHELSEA

Image
ALIJIUNGA na Real Madrid inayoshiriki La Liga, Julai Mosi,2019 akitokea Klabu ya Chelsea inayoshiriki Ligi Kuu England, anaitwa Eden Hazard na mkataba wake unatarajiwa kumeguka Juni 30,2024. Umri wake ni miaka 30, alizaliwa Januari 7,1991 ni raia wa Ubelgiji, anaimudu vema nafasi ya kiungo mshambuliaji na alikabidhiwa jezi namba 7 iliyowahi kuvaliwa na Cristiano Ronaldo alipokuwa akivaa uzi wa Real Madrid. Akiwa ndani ya Chelsea alicheza jumla ya mechi 245 ilikuwa kuanzia msimu wa 2012/2019 rekodi zinaonyesha kwamba alitupia mabao 85. Hayo ni mafanikio makubwa kwa kiungo huyo akiwa katika timu moja inayoshiriki ndani ya Ligi Kuu England. Akiwa ndani ya uzi wa Real Madrid amecheza jumla ya mechi 33 huku akiwa ametupia jumla ya mabao manne.Maisha yake yamekuwa tofauti na matarajio ya mashabiki wengi kwa kuwa amepoteza ule ufalme wake aliokuwa nao Chelsea.  Ni amecheza timu tofauti ikiwa ni pamoja na Lille inayoshiriki Ligue 1 aliweza kutwaa mataji tofautitofauti yaliyomfanya aw

VIDEO: SAA 840 ZA HAJI MANARA NJE YA SIMBA

Image
LEO Agosti 30, Ofisa Habari wa Yanga, Haji Manara anatimiza siku 30 ambazo ni saa 840 akiwa nje ya Simba baada ya kubwaga manyanga Julai 28 na hii ni rekodi yake katika ulimwengu wa Instagram ya hivi karibuni.  

TAIFA STARS KAZI INAENDELEA

PETER BANDA AITWA TIMU YA TAIFA YA MALAWI

Image
 BAADA ya kumaliza maandalizi ya kwanza kuelekea msimu mpya wa 2021/22 na kurejea Tanzania, kiungo  wa Simba  Peter Banda ameitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Malawi. Simba inayonolewa na Kocha Mkuu, Didier Gomes iliweka kambi kwa muda nchini Morocco kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya. Banda ameitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Malawi kwa ajili ya kujiandaa na michezo ya kuwania kufuzu Kombe la Dunia nchini Qatar mwaka 2022.  Pia wapo nyota wengine wa Simba ambao wapo kwenye kambi ya timu ya taifa ya Tanzania ambao ni pamoja na Aishi Manula, Shomari Kapombe, Mohamed Hussein pamoja na John Bocco.

VIDEO:JULIO AWAPONGEZA YANGA KWA SHUGHULI YA WIKI YA MWANANCHI

Image
JULIO amewapa pongezi Yanga kwa kufanya tamasha lao jana Agosti 29, Uwanja wa Mkapa ambalo liliwakusanya mashabiki wengi kutoka Tanzania na ilicheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Zanaco na ubao ulisoma Yanga 1-2 Zanaco.  

MKUDE APEWA MASHARTI SIMBA

Image
  K OCHA Mkuu  wa Simba,  Didier Gomes  amemuwekea  ngumu kiungo mkabaji wa  timu hiyo, Jonas Mkude  kwa kumtaka abadilike  juu ya matukio yake ya  utovu wa nidhamu kwa  kumpa onyo kali pamoja  na kumuweka chini ya  uangalizi wake. Mkude ambaye mwishoni  mwa msimu uliopita,  aliingia katika mzozo na  benchi la ufundi la timu  hiyo pamoja na wachezaji  wenzake kutokana na  kufululiza kwa matukio  yake ya utovu wa nidhamu  kiasi cha uongozi wa timu  hiyo kumsimamisha kwa  muda hadi kupelekwa  kwenye Kamati ya Nidhamu  ya Simba chini ya Kamanda  mstaafu wa Dar es Salaam,  Seleman Kova.   Taarifa za uhakika kutoka  ndani ya Simba, zinaeleza  kuwa Gomes ameamua  kumuweka chini kiungo  huyo na kumpa masharti  yake ikiwa atahitaji kuendelea  kucheza Simba.   Mtoa taarifa huyo  alienda  mbali zaidi kwa kusema  Gomes alitoa masharti  hayo kwa kuwa hataki  kuwagawa wachezaji wake  kupitia matatizo ya utovu wa  nidhamu kwani mipango yake  ni kishughulikia kwenye levo  moja. “Ni kweli

VIDEO: MWINYI ZAHERA AIPA TANO YANGA, AMCHAMBUA BANGALA

Image
MWINYI Zahera ambaye aliwahi kuwa Kocha Mkuu wa Yanga ameweka wazi kwamba ingizo jipya ndani ya Yanga, Bangala ni moja ya wachezaji wazuri ambao wamejiunga na Yanga kwa ajili ya msimu wa 2021/22.   

HAJI MANARA ANUSURIKA NA AJALI MBAYA YA GARI USIKU

Image
BAADA ya jana, Yanga kukamilisha kilele cha Wiki ya Mwananchi, Ofisa Habari wao Haji Manara muda wa kurejea nyumbani anasema kuwa alipata ajali mbaya ya gari. Manara ambaye aliibuka Yanga akitokea Simba leo alikuwa na mahojiano na kituo cha E FM jambo ambalo limemfanya akwame kufika katika kituo hicho kwa ajili ya mahojiano. Kupitia Ukurasa wake wa Instagram, Haji Manara aliweza kuwajibu E FM baada ya kuandika taarifa yenye kichwa cha habari, "Haji Haji'.  Kupitia Ukurasa wake Rasmi wa Istagram, Manara ameandika:" Ndugu zangu EFM  nawaomba radhi sana kwa kutofika kwenye kipindi asubuhi ya leo kama nilivyoahidi kwa sababu zilizo nje ya uwezo wangu. "Usiku wa jana nilinusirika na ajali mbaya ya gari baada ya gari yangu kugongwa vibaya na kusababisha kuharibika vibaya gari yangu. "Hadi kuja kulala ilikuwa ni mida mibaya ya usiku mkubwa na sikuweza kuamka mapema ili niwahi kipindi chenu alfajiri ya leo saa kumi na Mbili. "Nawaomba tena radhi nyie na