Posts

Showing posts from June, 2020

BARCELONA NI MWENDO WA SARE, MESSI AFIKISHA MABAO 700

Image
LIONEL Messi, staa ndani ya Klabu ya Barcelona usiku wa kuamika leo alifunga bao moja kwenye sare ya kufungana mabao 2-2 na Atletico Madrid Uwanja wa Nou Camp kwenye La Liga na kufikisha jumla ya mabao 700. Raia huyo wa Argentina anayekipiga pia kwenye timu ya taifa alifunga bao hilo kwa penalti kwa kupiga penalti ya panenka iliyozama ndani ya nyavu na kumshinda mlinda mlango wa Atletico Madrid, Jan Oblak. Messi ametoka kutoka kwenye jumla ya mabao 699 aliyokuwa nayo kibindoni baada ya kufunga bao mbele ya Leganes wiki mbili zilizopita na alishindwa kufurukuta kwenye mechi tatu zilizopita ikiwa ni mbele ya Sevilla, Athletic Bilbao na Celta Vigo kabla ya kuibuka mbele ya Atletico na kufunga bao hilo. Nyota huyo mwenye miaka 33,anaongoza kwa kutupia ndani ya Barcelona akiwa amefunga jumla ya mabao 630 kwenye timu yake huku akitupia jumla ya mabao 70 kwenye timu yake ya taifa ya Argentina. Mabao ya Barcelona yalifungwa na Diego Costa aliyejifunga dk 11 na Messi alifunga bao lake la

DI MARIA: BARCELONA WALITAKA KUNISAJILI KITAMBO

Image
Kiungo wa Klabu ya PSG, Angel Di Maria amesema kuwa Barcelona walitaka kumsajili 2017. Ubora wa kiungo huyo umezivutia timu nyingi ambazo zinahaha kupata saini yake ikiwa ni pamoja na Barcelona. Di Maria amesema kuwa Barcelona walimfuata 2017 ila aligoma kusaini dili lao kwa kuwa Klabu ya PSG iligoma kumruhusu. "Barca walijaribu kunisajili lakini mwisho wa siku klabu zote zilijadili na PSG ikagoma kuniruhusu kuondoka," amesema.

POLISI TANZANIA WATAJA NAFASI WANAYOITAKA NA MIPANGO YAO NDANI YA LIGI KUU BARA

Image
MALALE Hamsini, Kocha Mkuu wa Polisi Tanzania ya Kilimanjaro amesema kuwa malengo makubwa ya timu yake ni kuhakikisha wanamaliza Ligi Kuu Bara wakiwa nafasi ya nne. Malale amesema kuwa kikosi chake kipo tayari kwa ushindani na anaamini kwamba wachezaji wake watampa matokeo mazuri kwenye mechi zake zilizobaki. "Ushindani ni mkubwa hilo lipo wazi ila chochote kinaweza kutokea katika ligi nasi hatujakata tamaa bado tunapambana ili kuona namna gani tunafikia malengo yetu. "Tunahitaji kumaliza ligi tukiwa nafasi ya nne na hili linawekezekana kwa kufanya kazi kwa juhudi kwa mechi zetu zote zilizobaki," amesema. Polisi Tanzania ipo nafasi ya sita baada ya kucheza mechi 32 kibindoni ina pointi 47. Mechi yao iliyopita ya Ligi Kuu Bara walipotezwa na Mbao FC inayonolewa na Fekix Minziro kwa kufungwa bao 1-0 Uwanja wa CCM Kirumba. Imebakiza mechi sita mkononi ambazo ni sawa na pointi 18 ikiwa itashinda zote mfululizo bila kuyeyusha hata pointi moja zitawafanya wafikishe

VITA YA MABINGWA LEO TAIFA, ATAKAYEPENYA KUKUTANA NA BALAA LA YANGA

Image
LEO wakali wawili watakuwa uwanjani, Azam FC ambao ni mabingwa watetezi wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Simba ambao wao ni mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara. Kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho hatua ya robo fainali wanaume 22 watapambana ndani ya uwanja kusaka tiketi ya kutinga hatua ya nusu fainali. Mchezo wa leo unatarajiwa kuwa na hisia kubwa hasa ukizingatia kwamba tayari watani wa jadi wa Simba, Yanga wanasubiri mshindi tu wakutane naye. Kila timu inauhitaji mkubwa leo kushidia ili kukutana na Yanga ambayo iliishinda Kagera Sugar, Uwanja wa Taifa kwa kuifunga mabao 2-1. Azam FC iliyo chini ya Kocha Mkuu, Aristica Cioaba leo inahitaji kulipa kisasi cha kufungwa mechi mbili zote za Ligi Kuu Bara walipokutana na Simba huku Simba ikihitaji heshima pekee. Kwa upande wa wakali wa kucheka na nyavu Azam FC wanaye Obrey Chirwa ambaye ni namba moja kwa utupiaji Azam FC. Ametupia mabao nane na pasi tatu kwenye ligi. Simba wao wanaye Meddie Kagere ambaye ametupia mabao 19 na pasi

KADI NYEKUNDU YA AWESU AWESU YAMSHANGAZA NDANI YA UWANJA, AFUNGUKA MCHEZO ULIVYOKUWA

Image
KIUNGO wa Klabu ya Kagera Sugar, Awesu Awesu amesema kuwa hajui sababu ya kupewa kadi ya pili ya njano iliyomfanya atolewe nje jumla kwenye mchezo huo kwa kadi nyekundu. Yanga jana iliikaribiisha Kagera Sugar kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho hatua ya robo fainali ambapo Kagera Sugar ilipoteza kwa kufungwa mabao 2-1. Bao pekee la Kagera Sugar lilifungwa na Awesu Awesu dakika ya 19 huku yale ya yanga yakijazwa kimiani na David Molinga dakika ya 52 na lille la ushindi likipachikwa kimiani na Deus Kaseke kwa mkwaju wa penalti. Awesu alionyeshwa kadi mbili za njano jambo lililofanya aonyeshhwe kadi nyekundu na mwamuzi wa kati jambo ambalo amesema kuwa hatambui sababu ya yeye kuonyeshwa kadi hizo. Awesu amesema:"Sikuongea jambo lolote kadi ya kwanza nikishangaa namna nilivyopewa nikasema sawa, kadi ya pili nilikuwa nimechezewa faulo nikawa namtoa mchezaji mwenzangu maana nilishajua amepanic nashangaa nakutana na kadi nyingine sijui ilikuaje, sijaongea jambo lolote na wala sija

SERGIO RAMOS BONGE MOJA YA BEKI NA MAKADI YAKE KIBAO KIBINDONI

Image
SERGIO Ramos, beki anayekipiga ndani ya Klabu ya Real Madrid anatajwa kuwa miongoni mwa mabeki bora ambao wanacheza mpira kwa sasa duniani. Beki huyo amekuwa kwenye ubora wake kwa muda mrefu huku ikielezwa kuwa yeye ndiye ameshika ufunguo wa ubingwa wa La Liga kwa msimu huu wa klabu hiyo ambayo inapambania kombe vikali na Barcelona. Ndani ya uwanja amekuwa na rekodi nyingi nzuri ila mbali na kuwa bora ana rekodi ya kuwa mchezaji aliyeonyeshwa kadi nyingi uwanjani. Kibindoni ana jumla ya kadi 187  ambazo ameonyeshwa kwenye maisha yake ya soka akiwa kwenye harakati za kupambana. Ambapo ameonyeshwa jumla ya kadi 167 za njano na 20 nyekundu hiyo ni ndani ya La Liga pekee.

MORRISON AWAKIMBIZA MAKOMANDOO YANGA USIKU, BALAA LA SIMBA ACHA,NDANI YA CHAMPIONI JUMATANO

Image
MUONEKANO wa Ukurasa wa mbele Gazeti la Championi Jumatano

BERNARD MORRISON NI PASUA KICHWA NDANI YA YANGA, ATIMKA

Image
INAELEZWA kuwa kiungo mshambuliaji wa Yanga, Bernard Morrison ametoroka kambini jana wakati wachezaji walipokuwa wakijiaandaa na mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Kagera Sugar. Kwenye mchezo huo Morrison hakuwa sehemu ya mchezo ambapo Yanga iliibuka kidedea kwa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Kagera Sugar. Morrison amekuwa kwenye mvutano mkubwa na uongozi wa Yanga kwa sasa ambapo ishu kubwa inaeelezwa kuwa ni kuhusu mkataba wake ambao kila mmoja anasema jambo lake. Uongozi wa Yanga unasema kuwa Morrison ana kandarasi ya miaka miwili huku mchezaji mwenyewe akieleza kuwa ana mkataba wa miezi sita ambao unameguka msimu utakapoisha. Habari zinaeleza kuwa wakati wachezaji wakiwa kambini huku ulinzi ukiwa ni mkali Morrison alimua kusepa na alipobanwa aliwazidi ujanja walinzi na kusepa zake kuendelea na mipango yake mingine.  Morrison ametupia jumla ya mabao matatu na ana pasi tatu ndani ya ligi huku kwenye Kombe la Shirikisho akiwa ametupia bao moja.

ISHU YA OKWI KUREJEA SIMBA IMEIVA

Image
NYOTA wa zamani wa Klabu ya Simba, Emanuel Okwi inaelezwa kuwa yupo njiani kurejea ndani ya Klabu ya Simba ambayo aliitumikia msimu wa 2018/19 wakati wakitwaa ubingwa kwa mara ya pili mfululizo. Okwi amekuwa na mahusiano mazuri na Kagere ndani ya Simba pamoja na wachezaji wengine ikiwa ni pamoja na Clatous Chama ambaye ni kiungo kipenzi cha mashabiki wa Simba. Habari kutoka ndani zinaeleza kuwa tayari mchezaji huyo amekubali kurejea ndani ya Simba ili kuendelea kufanya kazi aliyoimaliza msimu wa 2018/19 wakati alipoibukia nchini Misri. Raia huyo wa Uganda ambaye anavaa jezi namba 7 hata kwenye timu ya Taifa ya Uganda mgongoni kwa sasa anaitumikia Klabu ya Al Ittihad ya Misri. "Yupo njiani kurejea ndani ya Simba na kila kitu kipo sawa ni suala la kusubiri tu mambo yakamilike ili atue tena Simba," ilieleza taarifa hiyo. Hivi karibuni Mtendaji Mkuu wa Simba, Senzo Mazingisa alisema kuwa mpango wa kusajili unategemea ripoti ya Kocha Mkuu, Sven Vandenbroeck.

KIKOSI BORA CHA LIGI KUU BARA NI NDANI YA CHAMPIONI JUMATANO

Image
KESHO ndani ya Championi Jumatano, usikubali kukosa nakala yako

MOLINGA, KASEKE WAKIWASHA TAIFA WAKIIMALIZA KAGERA SUGAR MABAO 2-1, AWESU MUACHE KABISA

Image
YANGA leo imefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 mbele ya Kagera Sugar kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho uliochezwa Uwanja wa Taifa. Kagera Sugar inayonolewa na Mecky Maxime itajilaumu yenyewe kipindi cha kwanza kwa kushindwa kutulia na kutumia nafasi ambazo walizitengeneza kwani walikuwa kwenye ubora upande wa kiungo wakiwapoteza mazima wachezaji wa Yanga. Bao la Kagera Sugar lilipachikwa kiufundi na nyota wao Awesu Awesu mwenye rasta kichwani ambaye alifunga akiwe nye kidogo ya 18 akimalizia pasi ya kisigino ya Yusuph Mhilu dakika ya 19. Yanga walikwenda mapumziko wakiwa nyuma kwa bao 1-0 ambapo kipindi cha pili walifanya mabadiliko kwa kumtoa Ditram Nchimbi na nafasi yake ikachukuliwa na Mrisho Ngassa mwamba wa ziwa Victoria mzee wa enjoi soka. Dakika ya 52 Molinga alifunga bao la kuweka usawa akimalizia pasi ya kichwa ya Ngassa naye akifunga bao la kichwa na kuwarudisha mchezoni Yanga. Katika harakati za Kagera Sugar kutaka kufunga, Awesu alionekana amechezewa faulo

NAMUNGO HAO WATINGA HATUA YA NUSU FAINALI, MAKANG'A ATUPIA BONGE MOJA YA BAO

Image
TIMU ya Namungo FC inayofundishwa na Kocha Mkuu, Hitimana Thiery, leo, Juni 30, imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 mbele ya Alliance FC kwenye mchezo wa hatua ya robo fainali uliochezwa Uwanja wa Majaliwa, Lindi. Ushindi huo unaifanya Namungo FC kukata tiketi ys kushirki hatua ya nusu fainali kwenye mchezo w Kombe la Shirikisho ambapo wanamsubiri mshindi wa mchezo kati ya Sahare All Stars atakayemenyana na Ndanda FC, kesho. Mabao ya Namungo yalipatikana kupitia kwa Bigirimana Blaise dakika ya 40 kwa mkwaju wa penalti baada ya mchezaji wa Alliance kunawa mpira ndani ya 18. Bao la pili lilipatikana kupitia kwa George Makang'a ambaye alibinuka akiwa ndani ya 18 na kufunga bao matata dakika ya 82 kwa pasi ya Hashim Manyanya. Ushindi huo unafanya Namungo kushusha presha ya kwanza kwenye hatua ya robo fainali na kuanza kuivutia kasi hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo mikubwa. Bingwa mtetezi wa taji la Shirikisho kwa sasa ni Azam FC iliyo chini ya Kocha Mkuu, Aristica Cioaba amba

MINZIRO ATAMBA KUWA ANGEANZA KUINOA MBAO MAPEMA ISINGEKUWA KWENYE PRESHA YA KUSHUKA DARAJA

Image
FELIX Miziro, Kocha Mkuu wa Mbao FC amesema kuwa angekuwa kwenye kikosi hicho tangu awali timu hiyo isingepata tabu ya kuwa  kwenye presha ya kushuka daraja. Mbao FC ilikuwa inanolewa na Kocha Mkuu, Hemed Morroco ambaye alibagwa manyanga kwa kile alichoeleza kuwa ni kutoridhika na matokeo aliyokuwa akiyapata kutokuwa mazuri. Kwa sasa Minziro amekabidhiwa timu ambapo ameingoza kwenye mechi mbili ambazo ni dakika 180 na amesepa na pointi sita na mabao mawili. Mchezo wake wa kwanza aliitungua Coastal Union ya Juma Mgunda bao 1-0 kisha akamalizana na Polisi Tanzania kwa kuifunga bao 1-0. Licha ya kushinda pointi zote sita anabaki nafasi ya 19 akiwa na pointi 29 kibindoni. Minziro amesema:"Ningekuwa na timu hii tagu awali nina amini kwamba tungekuwa mbali, tusingekuwa hapa tulipo ila hamna namna kwa kuwa nipo wakati huu nina kazi ya kufanya ili kuona timu inabaki kwnye ligi. "Ushindani ni mkuhwa na nilipopewa kikosi nilianza kuwanyoosha kwanza wachezaji ndio maana tulianza

UONGOZI WA SIMBA WAIPIGIA HESABU NDEFU AZAM FC KESHO TAIFA

Image
UONGOZI wa Simba umesema kuwa unautazama mchezo wa kesho wa hatua ya robo fainali kwa upekee licha ya wachezaji wake kutoka kupambana mechi mbili mfululizo nje ya Dar es Salam. Simba ilicheza mechi mbili Mbeya ambapo ilianza kumenyana na Mbeya City Uwanja wa Sokoine na ilishinda mabao 2-0 kisha ikamalizana na Tanzania Prisons kwa kulazimisha sare ya bila kufungana. Ikiwa tayari imeshatangazwa kuwa mabingwa, jana ilirejea kutoka Mbeya na leo imeanza maandalizi ya mchezo wao dhidi ya Azam FC utakaochezwa kesho Uwanja wa Taifa. Akizungumza na Saleh Jembe, Kocha Mkuu wa Simba, Sven Vandenbroeck amesema kuwa anatambua utakuwa mchezo mgumu ila wachezaji wake wapo tayari. "Ni mchezo mgumu kwetu na utakuwa na ushindani mkubwa hilo lipo wazi lakini nasi tumejipanga kuona namna gani tutapata matokeo mazuri. "Tumetoka kucheza mechi mbili hivi karibuni ambazo zilikuwa ni ngumu kwetu licha ya kwamba tumeshafanikisha lengo la kutwaa ubingwa bado tunahitaji kushinda mbele ya Azam FC,

ANGALIA SIMBA ILIVYOBEBA KWA UBINGWA WA GD TU, JIFUNZE…

Image
Na SALEH ALLY SIMBA amekuwa bingwa tangu juzi Jumamosi ingawa wengi hawakuwa wameling’amua hili mapema kwa kuwa walisubiri kuiona ikicheza mechi yake ya jana dhidi ya Prisons ya Mbeya. Kikosi cha Simba kilikuwa jijini Mbeya kikisubiri mechi hiyo ili kutangaza ubingwa rasmi kwa kuwa awali ilihitajika pointi tatu tu kumaliza kazi. Hii ilikuwa imeaminika hivyo, kiuhalisia, Simba ilihitaji pointi moja tu kutoka Mbeya baada ya mechi za jana lakini hata bila ya hiyo pointi moja, tayari ilishakuwa bingwa. Mambo yalikuwa hivi, hapa tunaweza kujifunza umuhimu wa mabao ya kufunga na kufungwa katika mchezo wa soka na namna Simba ilivyokuwa bingwa kupitia Goal Difference (GD). Nimesema Simba ilikuwa bingwa tangu juzi Jumamosi na ilichukua ubingwa kupitia GD ikiwa ni mara ya Azam FC kutoka sare ya mabao 1-1 dhidi ya Biashara United na Yanga wakashinda kwa mabao 3-2 dhidi ya Ndanda FC. Angalia, baada ya sare ya Azam FC na Biashara, Azam FC ikafikisha mechi 32 na pointi 59,

PUPA NA KUKOSA WATAALAMU SAHIHI, KUMEIFIKISHA YANGA HAPA KATIKA USAJILI

Image
NA SALEH ALLY TIMU ya Yanga ni kati ya zile kubwa na kongwe zaidi hapa nchini. Hii ni kati ya timu zile za mwanzoni kabisa kwenye historia ya soka hapa nchini na imefanikiwa kuufanyia kazi ukongwe wake kwa kuwa ndiyo kinara wa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara. Hii ni sifa ambayo huwezi kuiondoa kwao, labda iibuke timu nyingine na kuwapiku ingawa linaonekana kuwa ni jambo ambalo linaweza kuchukua muda kidogo. Ni timu ambayo inatajwa kuwa na mashabiki wengi zaidi hapa nchini, wenyewe wanaiita timu ya wananchi, lakini kwa misimu mitatu sasa, Yanga hii imeshindwa kufanya mambo makubwa ambayo yamekuwa yakisubiriwa na mamilioni ya mashabiki wao. Huu ni msimu wa tatu, Yanga wanaukosa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara na kibaya zaidi ni kwamba mara zote ubingwa huo unakwenda kwa watani wao wa jadi Simba. Hili limekuwa jambo ambalo linawaumiza sana mashabiki hao wa Jangwani, lakini hawana la kufanya kwa kuwa soka siku zote lazima liwe na mshindi, hata kama mtafanyaje

HIKI HAPA KIKOSI CHA YANGA KITAKACHOANZA LEO DHIDI YA KAGERA SUGAR UWANJA WA TAIFA

Image
Metacha Mnata Juma Abdul Jafary Mohamed Lamine Moro Said Juma Makapu Abdulaziz Makame  Deus Kaseke Feisal Salum David Molinga Haruna Niyozima Ditram Nchimbi SUB Farouk Shikhalo Adeyum Saleh Kelvin Yondani Raphael Daud Mrisho Ngassa Patrick Sibomana Tariq Seif

YANGA: TUNAIFUNGA KAGERA SUGAR NA TUNACHUKUA FA

MANCHESTER UNITED YAGOMA KUTOA DAU KUBWA KUMPATA SANCHO

Image
MANCHESTER United, imesema kuwa haipo tayari kutoa dau la zaidi ya paundi milioni 50 kupata saini ya Jadon Sancho anayekipiga ndani ya Borussia Dortmund. Klabu yake ya Ujerumani inahitaji dau la paundi milioni 100 ili wamuachie nyota huyo raia wa England mwenye miaka 20. Licha ya United iliyo chini ya Kocha Mkuu, Ole Gunnar Solskjaer kuitaka saini yake yupo tayari kumkosa nyota huyo kwa msimu ujao iwapo dau lake halitapungua. Nyota huyo anayevaa jezi namba saba mgongoni alijiunga na Dortmund msimu wa 2017 akitokea Klabu ya Manchester City amecheza jumla ya mechi 78 na kutupia mabao 30. Kwa msimu huu amefunga jumla ya mabao 20 na kutoa pasi 19 kwenye jumla ya mashindano yote msimu huu.

SIMBA YAIPANGIA AZAM FC KIKOSI KAZI NAMNA HII

Image
IKIWA kesho wanakutana kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho hatua ya robo fainali, Uongozi wa Simba umepanga kikosi kazi cha Azam FC ambacho ni hatari kikiwa uwanjani.  Simba itamenyana na Azam FC Uwanja wa Taifa majira ya saa 1:00 usiku. Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara kupitia Ukurasa wake wa Instagram amewapanga namna hii huku akisema kuwa hajatazama wale ambao wapo nje ya nchi kutokana na 'loc down':-Razack Abarola amemuweka langoni. Agrey Morris amesema kama ana miaka 20 hivi  Yakub Mohamed  Mudhathir Yahaya amesema ni mpiganaji uwanjani Salum Abubakar, 'Sure Boy' amesema ni mpiga pasi bora. Idd Kipagwile  Idd Naldo mtihani mkubwa  Obrey Chirwa  Shaban Chilunda

ALLIANCE KAZI KUBWA LEO NA NAMUNGO ROBO FAINALI

Image
TIMU ya Alliance FC, leo inamenyana na Klabu ya Namungo kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho hatua ya robo fainali. Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa leo Uwanja wa Majaliwa majira ya saa 10:00 huku ushindani ukitarajiwa kuwa mkubwa. Alliance FC inayonolewa na Kocha Mkuu Kessy Mzirai inakutana na mpinzani wake Namungo iliyo chini ya Kocha Mkuu, Hitimana Thiery. Hatua hii ya robo fainali mshindi atakayeshinda atakutana na mshindi wa mchezo kati ya Sahare All Stars na Ndanda FC. Bingwa wa michuano ya Kombe la Shirikisho ataiwakilisha nchi kwenye michuao ya kimataifa ya Kombe la Shirikisho. Bingwa mtetezi wa taji hilo ni Azam FC inayonolewa na Kocha Mkuu, Aristica Cioaba.

YANGA YAPANIA KULIPA KISASI KWA KAGERA SUGAR TAIFA

Image
KOCHA Mkuu wa Yanga,  Luc Eymael amesema kuwa anaamini wachezaji wake watalipa kisasi cha kufungwa mabao 3-0 na Kagera Sugar kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara walipokutana mara ya kwanza Uwanja wa Uhuru. Mchezo huo wa Ligi ulichezwa Januari 15,2020 ulikuwa ni wa kwanza kwa Eymael kukaa kwenye benchi la ufundi akichukua nafasi ya Mwinyi Zahera. Akizungumza na Saleh Jembe, Eymael amesema kuwa ana waamini vijana wake watalipa kisasi kwenye mechi ya leo hatua ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho ambalo ni muhimu kwao. "Walitufunga mchezo uliopita kwenye ligi ila sio huku kwenye Shirikisho, wachezaji wangu wapo vizuri na ninaamini watatumia nafasi ya kulipa kisasi ili kuendelea kulinda heshima ya uwezo wao," amesema. Mshindi wa mchezo wa leo atakutana na mshindi wa mchezo kati ya Simba na Azam FC hatua ya nusu fainali.

HAPA NDIPO ILIPO MTIBWA SUGAR

Image
MTIBWA Sugar iliyo chini ya Kocha Mkuu,  Zuber Katwila ikiwa imecheza jumla ya mechi 32 kibindoni ina pointi 37. Safu yake ya ulinzi inayoongozwa na kinda Dickson Job imeruhusu jumla ya mabao 29 ya kufungwa. Safu ya ushambuliaji imetupia jumla ya mabao 25 na katika mabao hayo kiungo wao Abdulrahman Humud ametupia mabao mawili. Haikuanza msimu vizuri kutokana na ushindani ambao ilikuwa inakutana nao hasa baada ya kushinda Kombe la Mapinduzi visiwani Zanzibar. Ofisa Habari wa Mtibwa Sugar, Thobisa Kifaru amesema kuwa baada ya kushinda taji hilo kwa kuitungua Simba bao 1-0 wapinzani wao walikuwa wanawakamia. Kibarua chake kwa sasa ni kuweza kutetea nafasi yake ndani ya Ligi Kuu Bara kutokana na nafasi ambayo ipo kwa sasa kutokuwa salama. Katwila anaamini kwamba vijana wake wanaweza kurejea kwenye ubora taratibu na kuanza kupata matokeo chanya kwenye mechi zao zilizobaki.

EXCLUSIVE:MORRISON ASIMULIA ALIVYOCHOMWA SINDANO NNE KUIMALIZA SIMBA

Image

MOTO WA KUNDI A ACHA KABISA, CHEKI NAMNA VITA ILIVYO TAMU

Image
MSIMAMO wa Kundi A wa Ligi Daraja la Kwanza, vita kubwa ni nafasi ya kupanda daraja jumlajumla ambapo Dodoma FC na Ihefu zote zinalingana pointi tofauti yao ikiwa ni kwenye idadi ya mabao. Zote zimebakiwa na mechi mbili mkononi ili kumaliza mzunguko wa pili na kumpata mshindi, cheki ulivyo.

KAGERA SUGAR WAPO TAYARI KUPAMBANA NA YANGA KESHO TAIFA

Image
TIMU ya Kagera Sugar, kesho ina kazi ya kupambana na Klabu ya Yanga kwenye mchezo wa hatua ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho. Mchezo huo utapigwa majira ya saa 1:00 usiku unatarajiwa kuwa na ushindni mkubwa kutokana na kila timu kuhitaji kusonga mbele. Kocha Mkuu wa Kagera Sugar, Mecky Maxime amesema kuwa mpango mkubwa nikupata matokeo ili kusonga mbele kwenye hatua ya nusu fainali. Maxime ataingia uwanjani akiwa na kumbukukumbu ya kuwanyoosha Azam FC kwenye mchezo wa ligi uliochezwa Uwanja wa Kaitaba kwa bao 1-0. Yanga nao pia mchezo wao wa mwisho wa ligi Uwanja wa Taifa iliibuka na ushindi wa mabao 3-2 mbele ya Ndanda FC. Kwenye mchezo wa mzunguko wa kwanza kwenye ligi walipokutana Yanga na Kagera Sugar Uwanja wa Uhuru, Kagera Sugar iliibuka na ushindi wa mabao 3-0. Ulikuwa ni mchezo wa kwanza kwa Kocha Mkuu, Luc Eymael kukaa kwenye benchi la ufundi ndani ya Yanga akichukua mikoba ya Luc Eymael. Eymael amesema kuwa yupo tayari kwa ajili ya kupambana na Kagera Sugar kwan

VIDEO: KOCHA WA SIMBA AZUNGUMZIA KUHUSU MIPANGO YAKE, KESHO KUANZA MAZOEZI

Image

AZAM NAO KUKIWASHA USIKU DHIDI YA SIMBA, TAIFA

Image
AZAM FC, Julai Mosi, Uwanja wa Taifa itakuwa na kazi ya kumenyana na Simba kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho. Mchezo huo awali ulitarajiwa kuchezwa majira ya saa 10:00 Uwanja wa Taifa ila ratiba ya muda imebadilishwa. Taarifa iliyotolewa leo imeeleza kuwa muda wa mechi hiyo utakuwa ni saa 1:00 usiku ila tarehe itabaki kuwa ileile ya Julai Mosi. Azam FC inashuka uwanjani akiwa ni bingwa mtetezi wa taji hilo. Mshindi wa mchezo huo atamenyana na mshindi wa mchezo kati ya Yanga na Kagera Sugar hatua ya nusu fainali.