VIDEO:HUYU HAPA MO AKIZUNGUMZIA ISHU YA KUJIENGUA SIMBA,SABABU HIZI HAPA


MOHAMED Dewji, 'Mo', Mkurugenzi wa Bodi ya Wakurugenzi ndani ya Klabu ya Simba ameweka wazi kuwa kwa sasa atabaki kuwa Mwanahisa ndani ya timu hiyo baada ya kukubaliana na Bodi kwamba anaweza kustep down, (kukaa pembeni) kwenye nafasi hiyo. 
 
Mo amesema kuwa sababu kubwa ambayo imemfanya akajiengua ni kutokuwa na muda kwa kuwa amekuwa akisafiri mara kwa mara hivyo nafasi hiyo itakuwa mikononi mwa Salim Abdalah, 'Tryagain'. 

 Mo amebainisha pia mafanikio ambayo wameyapata kwa muda wa miaka minne ikiwa ni ile ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara mara nne pamoja na kuweza kufanya vizuri katika Ligi ya Mabingwa Afrika huku akisistiza kwamba bado anaipenda Simba na yupo Simba.

 



Comments

Popular posts from this blog

ISHU YA MORRISON KUHUSU MKATABA WAKE IPO MIKONONI MWA KAMATI YA SHERIA NA HADHI ZA WACHEZAJI

BREAKING: MASHABIKI RUKSA KWENDA UWANJANI, UTARATIBU WATAJWA

AFRICAN LYON WADAI KUWA WAZO LA VISIT TANZANIA NA LOGO MPYA YA SIMBA IMETOKA KWAO