Posts

Showing posts from July, 2021

TIMU YA TAIFA U 23 YAREJEA NA TAJI

Image
  KIKOSI cha timu ya taifa chini ya miaka 23 leo Agosti Mosi kimewasili Tanzania kikitokea nchini Ethiopia ambapo kimetwaa taji la Cecafa. Ushindi wa penalti 6-5 mbele ya Burundi uliwapa nafasi ya kutwaaa taji hilo. Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania, (TFF), Wallace Karia amesema kuwa ni jambo la furaha kwa ushindi waliopata. Mbali na Karia pia Katibu Mkuu wa TFF, Wilfred Kidao nao alikuwa miongoni mwa waliokuepo leo Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere. Mashabiki nao walijitokeza kwa ajili ya kuwapokea wachezaji hao ambao wameweza kuipeperusha vema bendera ya Tanzania. Wakiwa na ngoma zao mashabiki walipata pia muda wa kucheza na wachezaji wa U 23 pamoja na kupiga picha na kombe hilo nje ya uwanja kwa muda.

VIDEO: NAMNA MSHAMBULIAJI MPYA WA YANGA FISTON ALIVYOTUA BONGO

Image
LEO Julai 31 mabosi wa Yanga wamempokea mshambuliaji mpya Fiston Mayele ambaye amekuja kumalizana nao ili aweze kusaini dili jipya akitokea Congo.   

RONALDINHO MZEE WA KUKERA AMBAYE NI BALOZI WA BARCA

Image
 MIONGONI mwa wachezaji ambao rekodi zao ni bora ndani ya uwanja ni pamoja na raia wa Brazil anaitwa Ronaldo de Assis Moreira aliletwa duniani Machi 21,1980 ana umri wa miaka 41. Jina lake maarufu ni Ronaldinho Gaucho ama kifupi wengi hupenda kumuita Ronaldinho ambaye ni mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Brazil na kwa sasa ni balozi wa muda wote wa Klabu ya Barcelona. Amecheza jumla ya mechi 511 katika timu mbalimbali ambazo aliweza kucheza zama za maisha yake ya soka na alifunga jumla ya mabao 205.   Rekodi zinaonyesha kwamba alikuwa ndani ya Gremio msimu wa 1998/2001 ambapo alicheza jumla ya mechi 89 na alifunga mabao 47. Ni timu ya Barcelona hapo alicheza mechi nyingi zaidi ambazo ni 145 na alifunga mabao 70. Ndani ya Klabu ya Fluminens ya Brazil rekodi zinaonyesha kuwa msimu wa 2015 alicheza mechi chache kwa maisha yake ya soka ambazo zilikuwa ni 7 na hakupata bahati ya kutupia bao hata moja. Katika timu yake ya taifa ya Brazil rekodi zinaonyesha kwamba alicheza jumla y

KISA KAGAME CUP, AZAM WASHUSHA VIKOSI VIWILI

‘GUTY’ HUYOO SIMBA

KISA KESI YA CAS YANGA, MORRISON CAS WAINGIA KWENYE VITA YA TAMBO

USAJILI UNAHITAJI AKILI UKIZUBAA UNAPIGWA

Image
  TAYARI mambo yanazidi kupamba moto kwenye masuala ya usajili kwa ajili ya maandalizi ya msimu wa 2021/22. Bingwa ashajulikana ambaye ni Simba na zile nne ambazo zimeshuka zimefahamika. Anza na Ihefu pamoja na Gwambina hizi zilikuwa zina msimu mmoja wa kazi na mmoja umetosha kuwarejesha ambapo walikuwa huko Ligi Daraja la Kwanza. Kazi wanayo kwa ajili ya kuweza kurudi tena ndani ya ligi. Mwadui FC na  JKT Tanzania hawa walikuwepo muda kidogo lakini bahati haikuwa yao wanakazi nyingine ya kufanya kwa ajili ya kuweza kurudi ndani ya ligi. Kazi ni moja kwao kupambana kutimiza majukumu yao kwa kuwa wakati uliopo ni sasa na kikubwa ni maandalizi mazuri na kufanya kazi kwa ushirikiano. Mpaka sasa kwa timu ambazo zimejipanga kufanya usajili ninaona kwamba zimeweza kufanya kile ambacho zinahitaji jambo ambalo katika hilo sina mashaka nalo. Jambo la msingi ambalo linapaswa kuzingatiwa katika usajili ambao unafanywa ni kufuata ripoti ya mwalimu, yeye ndiye ambaye anajua kwamba anahitaji

VIDEO:TASWA WAKABIDHIWA KOMBE NA DStv

Image
TWASWA FC wakabidhiwa kombe kutoka Dstv Bonanza  

SAIDO AWAGAWANYA MABOSI YANGA, WENGINE WATAKA ASEPE MAZIMA

Image
  V IONGOZI wa  Yanga wamejikuta  wakiwa katika njia  panda mara baada  ya kupatwa na kigugumizi  cha kuachana au kubaki kwa  mshambuliaji wao, Saidi  Ntibazonkiza ‘Saido’. Ntibazonkiza alijiunga na  Yanga katika usajili wa dirisha  dogo uliofanyika Januari  2021 ambapo mpaka sasa  ameitumikia klabu hiyo kwa  nusu msimu.   Chanzo cha kuaminika  kutoka Yanga kimeliambia  Championi Jumamosi kuwa,  viongozi hao mpaka sasa  wameshindwa kutoa maamuzi  juu ya mchezaji huyo asalie  au aachwe ambapo wanaotoka  aondoke wametaja sababu ni  wingi wa idadi ya wachezaji  wa kimataifa ambao unahitaji  kuwasajili lakini pia ishu ya  majeraha ya mara kwa mara.   “Uongozi wa Yanga  unashindwa kuamua hatima  ya Saido kuwa asalie au  aondolewe, kama ambavyo  unamuona kuwa mchezaji huyo  chini ya kocha Nasreddine Nabi  ameshindwa kabisa kutamba  katika kikosi cha kwanza huku  mara nyingi akiwa katika  wachezaji wa akiba. “Lakini pia ishu ya majeraha  ya mara kwa mara ambayo  amekuwa akikumbana

NYOTA HAWA WAMEMALIZANA NA SIMBA, MMOJA AWAZIMIA SIMU YANGA

Image
  S IMBA  imeanza kwa  kasi harakati zake za  kusuka upya kikosi  chake kwa ajili ya Ligi  ya Mabingwa Afrika na Ligi  Kuu Bara msimu ujao, baada  ya kumalizana na nyota watatu  fasta. Simba imepania kufika fainali  ya Ligi ya Mabingwa msimu ujao  baada ya kuishia hatua ya robo  fainali msimu huu.   Wekundu hao wamemalizana  na kipa namba moja wa Tanzania  Prisons, Jeremiah Kisubi kwa  kumsainisha mkataba wa miaka  miwili kimyakimya. Prisons inayomilikiwa na Jeshi  la Magereza, juzi ilimsajili kipa  wa Mbeya City, Haroun Mandanda  baada ya kupata taarifa za Kisubi  kusaini Simba.   Simba imepanga kukifanyia  maboresho machache kikosi chao  katika kuhakikisha wanafanya  vema katika Ligi ya Mabingwa  Afrika. Kwa mujibu wa taarifa ambazo  imezipata  Championi Ijumaa,   Simba imefanikisha usajili wa  kipa huyo kwa ajili ya kumpa  changamoto Aishi Manula.   Mtoa taarifa huyo alisema kuwa  Simba ilifanikisha usajili wa kipa  huyo haraka mara baada ya Ligi  Kuu Bara kumalizika kwa k

RASTA HUYU KUTOKA ZAMBIA MKALI WA KUKABA KUTUA YANGA

Image
  T ETESI za usajili  Yanga zinasema  kuwa, timu hiyo  ipo katika hatua  za mwisho za kukamilisha  usajili wa beki wa Zesco ya  nchini Zambia, Mkongomani  Marcel Kalonda ambaye  anatumia guu la kushoto  na ni mkali katika kukaba  katika ile staili ya mtu na  mtu ‘man to man’.   Uwezo wake huo unaweza  kuwa kikwazo kwa viungo  wasumbufu kwenye ligi  kama Clatous Chama, Luis  Miquissone pamoja na  mastaika kama John Bocco na  Prince Dube.   Kalonda, 23, mkataba  wake na Zesco unatarajiwa  kumalizika Desemba 31,  mwaka huu hivyo huenda  akaja kuchukua nafasi ya  Mghana Lamine Moro ambaye  tayari Yanga imetangaza  kuachana naye  Alhamisi. Yanga imepanga kukiboresha  kikosi chao ili kifanye vizuri  katika Ligi ya Mabingwa  Afrika.  Kwa mujibu wa taarifa  ambazo imezipata  Championi  Ijumaa,  kocha Nasreddine  Nabi ndiye anayetajwa  kupendekeza jina la beki huyo  mwenye uwezo mkubwa  wa kukaba, kupunguza na  kuanzisha mashambulizi  kwenye goli la wapinzani. “Katika kikao cha  Jumat

CORONA YAITIKISA MANCHESTER UNITED

Image
 MANCHESTER United imelazimika kusogeza mbele mchezo wao wa kirafiki dhidi ya Preston North End uliotarajiwa kuchezwa leo Jumamosi kutokana na kutikishwa na janga la Corona. Inaelezwa kuwa kuna wachezaji tisa wa Manchester United ambao wamepata Virusi vya Corona jambo ambalo limezua hofu na kuamua kuchukua tahadhari. Vipimo vilivyochukuliwa kufuatia mechi ya kirafiki ya juzi Jumatano dhidi ya Brenford ambayo ilichezwa mbele ya mashabiki 30,000, vilionyesha idadi hiyo ya waathirika katika kikosi hicho kinachonolewa na Kocha Mkuu, Ole Gunnar Solkjaer. Mechi hiyo ya Jumatano iliisha kwa sare ya kufungana mabao 2-2. Pia mechi ya Bretford dhidi ya West Ham inaweza isichezwe kwa kuwa Brendford nao wanafanya vipimo kutokana na kuhusika na mchezo dhidi ya United. Taarifa kutoka United jana ilieleza kuwa kuendeleza usalama dhidi ya Corona ndiyo kipaumbele chao jambo ambalo limefanya waliopata Corona wajitenge na wengine. "Kufuatia vipimo vya wachezaji wa kikosi cha kwanza tumepata i

WASIOOA WAKWAMWA KWA WALIOOA, WANYOOSHWA 3-0, ZACHAPWA KAVUKAVU

Image
  TIMU ya Wasioa wameshindwa kufuta uteja mbele ya Walioa katika mchezo maalumu uliopigwa Ijumaa Julai 30, 2021 kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Dk Reginald Mengi, Dar huku wachezaji nguli wa Wasioa wakitaka kuzichapa kavukavu wenyewe kwa wenyewe.   Katika mchezo huo ambao ulihudhuriwa na mashabiki wengi wakiwemo wadhamini wa mchezo huo kutoka Smart Gin, Creative Bee ambao umemalizika kwa Wasioa kukubali kichapo cha mabao 3-0. Hii ni mara ya pili kwa Wasioa kukubali kichapo katika mchezo huo ambao umekuwa maalum kwa Wafanyakazi wa Kampuni ya Global Group huku ukishirikisha washirika wake mbalimbali.   Wachezaji wa Wasioa walianza kuwa watata baada ya mwamuzi kutoa faulo ambayo ilipelekea kushikana kati ya mchezaji wa Walioa, nahodha Philip Nkini na beki wa Wasio, Marco Mzumbe kabla ya kuamuliwa na wachezaji wengine akiwemo Musa Mateja aliyeamua kujipa ukocha baada ya timu yake kuona inalekea kubaya lakini hakuweza kusaidia chochote. Lakini hali ya kutoelewana kwa wachezaji wa

VIDEO: LUIS AKUBALI KUPATA CHANGAMOTO MPYA,KUIBUKIA MISRI

Image
IMEELEZWA kuwa Luis Miquissone yupo kwenye hesabu za kuwaniwa na Al Ahly ambapo wakala wa mchezaji huyo amebainisha kuwa kuna ofa ya bilioni mbili ambayo imetumwa Simba huku kiungo huyo akiwa tayari kupata changamoto mpya.   

SABABU ZA YANGA KUACHANA NA LAMINE MORO IPO HIVI

Image
  I METAJWA nidhamu ndiyo sababu  iliyomuondoa nahodha na beki wa kati wa  Yanga, Mghana, Lamine Moro kwenye  usajili wa msimu ujao. Hiyo ikiwa ni siku chache tangu, uongozi wa  Yanga utoe taarifa za kuachana na beki huyo mwenye  umbo kubwa.   Moro anaondoka Yanga akiwa amecheza michezo  21 katika Ligi Kuu Bara akifunga mabao 4 huku  akipiga asisti moja pekee. Mmoja wa mabosi wa Yanga, ameliambia  Championi Ijumaa, beki huyo hakuachwa na timu  hiyo kutokana na kiwango, bali nidhamu ndiyo  iliyomuondoa katika timu.   Bosi huyo alisema kuwa Moro hivi karibuni  alitofautiana na Kocha Mkuu wa timu hiyo, Nasreddine  Nabi katika suala la nidhamu kabla ya kuondoa  kambini Ruangwa, Lindi wakati Yanga inajiandaa na  mchezo dhidi ya Namungo FC. Aliongeza kuwa beki huyo alitenda utovu wa  nidhamu lakini akaonekana mgumu katika kuomba  msamaha kwa kocha huyo. “Uongozi wa Yanga umefikia uamuzi wa kuachana  na Moro baada ya kuitumikia kwa mwaka mmoja na  nusu huku akiwa mkali.