YANGA YAPENYA 16 BORA MBELE YA TANZANIA PRISONS


 UWANJA wa Nelson Mandela umeshuhudia kikosi cha Yanga kikisepa na ushindi kwa mara ya kwanza mbele ya Tanzania Prisons.

Mchezo wa leo ulikuwa ni wa Kombe la Shirikisho hatua ya 16 bora ambapo baada ya dakika 90, ubao ulisoma Prisons 0-1 Yanga.

Ni Yacouba Songne alipachika bao hilo la ushindi kipindi cha pili dakika ya 53 na kuipa kuwanyanyua mashambiki wa timu hiyo inayonolewa na Kocha Mkuu, Nassredine Nabi.

Mchezo wa kwanza ambao ulikuwa wa ligi walipokutana Uwanja wa Nelson Mandela timu zote ziligawana pointi mojamoja kwa kufunngana bao 1-1 zama za Cedric Kaze.

Baada ya mchezo huo, kiungo mshambuliaji wa Yanga, Saido Ntibanzokiza amesema kuwa kwao ni furaha kusonga mbele na ni ushindi wa timu nzima kiujumla.

"Tumepata ushindi ninafurahi naamini hii ni furaha ya wachezaji kiujumla pamoja na benchi la ufundi," amesema.



Comments

Popular posts from this blog

ISHU YA MORRISON KUHUSU MKATABA WAKE IPO MIKONONI MWA KAMATI YA SHERIA NA HADHI ZA WACHEZAJI

BREAKING: MASHABIKI RUKSA KWENDA UWANJANI, UTARATIBU WATAJWA

AFRICAN LYON WADAI KUWA WAZO LA VISIT TANZANIA NA LOGO MPYA YA SIMBA IMETOKA KWAO