KANE MAJANGA TUPU, HATIHATI KUUKOSA MCHEZO WA KUFUZU KOMBE LA DUNIA


 HARRY Kane, mshambuliaji wa kikosi cha Tottenham imeelezwa kuwa anaweza kukaa nje ya uwanja kwa muda mrefu tofauti na ilivyoelezwa awali.

Kane aliumia kwenye mchezo wa Ligi Kuu England dhidi ya Liverpool uliochezwa Alhamisi iliyopita ambapo timu yake ilifungwa mabao 3-1.

Taarifa zimekuwa zikisema kuwa mchezaji huyo anaweza kukosa mchezo wa timu ya Taifa ya England wa kufuzu Kombe la Dunia unaotarajiwa kuchezwa Machi mwaka huu 2021.

Kocha Mkuu wa Tottenham, Jose Mourinho amesema kuwa ni kweli mchezaji wake ameumia ila muda ambao atakaa nje ya uwanja bado hajatambua.

"Kweli Kane ameumia ila kuhusu majeraha yake na muda ambao atakosekana ni jambo ambalo linahitaji muda hivyo tusubiri na tuone," .



Comments

Popular posts from this blog

ISHU YA MORRISON KUHUSU MKATABA WAKE IPO MIKONONI MWA KAMATI YA SHERIA NA HADHI ZA WACHEZAJI

BREAKING: MASHABIKI RUKSA KWENDA UWANJANI, UTARATIBU WATAJWA

AFRICAN LYON WADAI KUWA WAZO LA VISIT TANZANIA NA LOGO MPYA YA SIMBA IMETOKA KWAO