ZIDANE: NILIMWAMBIA MARADONA KWAMBA NI MCHEZAJI BORA

 


ZINADINE Zidane, Kocha Mkuu wa Real Madrid amesema kuwa alipata bahati ya kuzungumza na Diego Maradona na alimwambia kwambe yeye ni aina ya wachezaji bora ndani ya uwanja.


Zidane amesema kuwa taarifa za kutangulia mbele za haki kwa gwiji huyo zilimshtua na kumfanya afikirie mambo mengi kuhusu uwezo wa Maradona.


Maradona alitangulia mbele za haki Novemba 25 akiwa nyumbani, Argentina ikiwa ni muda mfupi baada ya kutimiza miaka 60.


Zidane amesema:"Hakuwa mtu mwenye maneno mengi ila utendaji zaidi, nilipata bahati ya kuzungumza naye na nilimuambia kwamba yeye ni mchezaji bora na mwenye uwezo ndani ya uwanja.


"Kwa kuwa ametangulia basi hakuna namna imani ni kwamba uwezo wake utadumu kwenye mioyo ya wanafamilia ya michezo," .



Comments

Popular posts from this blog

ISHU YA MORRISON KUHUSU MKATABA WAKE IPO MIKONONI MWA KAMATI YA SHERIA NA HADHI ZA WACHEZAJI

BREAKING: MASHABIKI RUKSA KWENDA UWANJANI, UTARATIBU WATAJWA

AFRICAN LYON WADAI KUWA WAZO LA VISIT TANZANIA NA LOGO MPYA YA SIMBA IMETOKA KWAO