SIMBA YAPENYA MBELE YA WANAIGERIA LICHA YA VIKWAZO

 


KIKOSI cha Simba, leo Novemba 29 kimeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji wao Plateau United kwenye mchezo wa awali wa Ligi ya Mabingwa Afrika. 


Mchezo huo uliochezwa Uwanja wa New Jos, nchini Nigeria wenye uwezo wa kuchukua jumla ya mashabiki 40,000 ulikuwa na visa vingi kwa wenyeji wakiwa na lengo na kuwatoa Simba mchezoni.


Bao la ushindi limepatikana dakika ya 53 kupitia kwa Clatous Chama kwa pasi ya Luis Miquissone ambaye alikuwa ni mwiba kwa Plateau United.


Miongoni mwa vikwazo ambavyo walikuwa wanaweka watu wa Nigeria ni pamoja na kuwabugudhi waandishi wa Habari wa Tanzania katika kufanya ripoti ya matukia.


Pia jana, Novemba 28 licha ya jitihada za uongozi wa Simba kuomba matangazo yarushwe mubashara kupitia Azam Tv jamaa waligoma na kuweka ngumu mpaka leo siku ya mchezo Azam Tv hawakupewa haki ya kutangaza mubashara zaidi ya kutangaza kupitia kwa radio.


Habari nyingine ni kwamba Simba walipigwa mkwara kwenye upande wa kutumia wapishi wao mwanzo na kuleta ubishi mkubwa na pia wakazusha na ishu ya Corona kwa nyota wa Simba ikiwa ni kwa Claotous Chama, Luis, John Bocco lengo moja tu kuwatoa Simba mchezoni.


Ushindi walioupata Simba ugenini si haba ikiwa watapmbana kupata ushindi Uwanja wa Mkapa Desemba 6 na ikishinda itapenya mpaka hatua ya mtoano.



Comments

Popular posts from this blog

SIMBA NA YANGA MSIBEBE MATOKEO UWANJANI

FT: VPL:SIMBA 4-0 IHEFU

WAMEANZA NA MAJANGA MSIMU MPYA WA 2021/22, SIMBA WANAWEZA KUKOSA UBINGWA