NGORONGORO HEROES YATINGA FAINALI YA CECAFA KWA MBINDE




TIMU ya Taifa ya Tanzania ya Vijana chini ya umri wa miaka 20, Ngorongoro Heroes leo Novemba 30 imetinga hatua ya fainali ya mashindano ya Cecafa kwa mbide baada ya kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Sudani Kusini.


Mchezo wa leo ambao umechezwa Uwanja wa Black Rhino Academy Karatu ulishuhudia dakika 45 timu zote mbili zikienda kwenye vyumba vya kubadilishia nguo zikiwa zimetoshana nguvu.


Iliawachukua Ngorongoro Heroes dakika 10 kupata bao la uongozi kupitia kwa Kassim Haruna aliyepachika bao hilo dakika ya 55 baada ya beki wa Ngorongoro, David Kameta kutoa pasi kati iliyokutana na Kelvin John aliyeachia shuti likakutana na kipa aliyetema mpira uliokutana na Haruna.




Comments

Popular posts from this blog

SIMBA NA YANGA MSIBEBE MATOKEO UWANJANI

FT: VPL:SIMBA 4-0 IHEFU

WAMEANZA NA MAJANGA MSIMU MPYA WA 2021/22, SIMBA WANAWEZA KUKOSA UBINGWA