JIMENEZ AZUNGUMZIA HALI YAKE



MSHAMBULIAJI wa Wolves, Raul Jimenez amezungumza kwa mara ya kwanza kupitia twitter baada ya kufanyiwa upasuaji kutokana na mshtuko kwenye ubongo. 

Raia huyo wa Mexico amezungumza kwa mara ya kwanza  baada ya kufanyiwa upasuaji kwa kuwa alipata mshtuko alipogongana na David Luiz kwenye mchezo wa Ligi Kuu Engand Jumapili ambapo Arsenal ilipoteza kwa kufungwa mabao 2-1.

Nyota huyo amesema kuwa bado yupo kwenye matibabu na anaamini kwamba atarejea uwanjani hivi karibuni kwa kuwa anaendelea vizuri. 

Jimenez ameweka wazi kuwa shukrani zake ni kwa Mungu pamoja na mashabiki ambao wamekuwa wakimtumia ujumbe kwa ajili ya kumjulia hali na kumuombea kheri.

"Asante kwa sapoti kupitia meseji zenu mashabiki, nipo kwenye maendeleo mazuri kwa sasa na nina matumaini kwamba nitarejea uwanjani hivi karibuni," amesema.

Wolves pia wameweka taarifa kwamba nyota huyo anaendelea vizuri baada ya kufanyiwa upasuaji kwa kuwa ulikwenda vizuri katika hospitali ya London hivyo atarejea uwanjani hivi karibuni.





Comments

Popular posts from this blog

SIMBA NA YANGA MSIBEBE MATOKEO UWANJANI

FT: VPL:SIMBA 4-0 IHEFU

WAMEANZA NA MAJANGA MSIMU MPYA WA 2021/22, SIMBA WANAWEZA KUKOSA UBINGWA