SIMBA WAANZA KUPIGA MATIZI LEO KUIWINDA JKT TANZANIA

 


SIMBA leo wameanza mazoezi kwa ajili ya kujiwinda na mchezo wao wa Ligi Kuu Bara utakaopigwa Oktoba 4 Uwanja wa Jamhuri Dodoma dhidi ya JKT Tanzania.

Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara amesema kuwa kikosi kipo sawa na kinaendelea na programu za mwalimu ili kuweza kufikia malengo ambayo wamejiwekea.

"Leo tumeanza na mazoezi maalumu kwa ajili ya mchezo wetu dhidi ya JKT Tanzania, nina amini kwamba utakuwa mchezo mgumu lakini kwa kuwa sisi ni mabingwa lazima tujipange sawasawa.

"Kwa upande wa benchi la ufundi baada ya kutoka kushinda mbele ya Gwambina FC wao pia wapo sawa wanatambua kwamba mchezo wetu dhidi ya JKT Tanzania utakuwa na ushindani mkubwa, mashabiki watupe sapoti," amesema.


JKT Tanzania itamenyana na Simba ikiwa imetoka kupoteza kwa kufungwa mabao 3-0 mbele ya Polisi Tanzania Uwanja wa Ushirika, Moshi.



Comments

Popular posts from this blog

ISHU YA MORRISON KUHUSU MKATABA WAKE IPO MIKONONI MWA KAMATI YA SHERIA NA HADHI ZA WACHEZAJI

BREAKING: MASHABIKI RUKSA KWENDA UWANJANI, UTARATIBU WATAJWA

AFRICAN LYON WADAI KUWA WAZO LA VISIT TANZANIA NA LOGO MPYA YA SIMBA IMETOKA KWAO