KMKM WATIA TIMU DAR, KIINGILIO BUKU TANO TU

 



TIMU ya KMKM SC ya Zanzibar  imewasili leo Septemba 30 Dar tayari kwa mchezo wa kirafiki leo dhidi ya Yanga utakaochezwa Uwanja wa Azam Complex.

Mchezo huo wa kirafiki unatarajiwa kupigwa majira ya saa 1:00 usiku ukiwa na malengo ya kukiweka sawa kikosi cha Yanga kwa ajili ya mechi za Ligi Kuu Bara.

Mechi hiyo kiingilio cha 5,000 mzunguko na 10,000 VIP. 


Yanga inayonolewa na Kocha Mkuu, Zlatko Krmpotic ipo kwenye maandalizi ya mchezo wa ligi dhidi ya Coastal Union unaotarajiwa kuchezwa Oktoba 3, Uwanja wa Mkapa.



Comments

Popular posts from this blog

SIMBA NA YANGA MSIBEBE MATOKEO UWANJANI

FT: VPL:SIMBA 4-0 IHEFU

WAMEANZA NA MAJANGA MSIMU MPYA WA 2021/22, SIMBA WANAWEZA KUKOSA UBINGWA