MANCHESTER CITY KUTOA WACHEZAJI WATATU KUMPATA MESSI

 


MAN City imeripotiwa kuwa ipo tayari kuipa Barcelona pauni milioni 89.5 pamoja na wachezaji watatu; Bernardo Silva, Gabriel Jesus na Eric Garcia ili kumpata supastaa Lionel Messi.

 

City wanamatumaini makubwa ya kufikia makubaliano na Barcelona baada ya Messi kutangaza hivi karibuni juu ya nia yake ya kuondoka Camp Nou katika kipindi hiki cha usajili.

 

Kama Messi akikubaliana na City, ataungana tena na kocha wake wa zamani Pep Guardiola baada ya miaka yake ya mafanikio Nou Camp akifunga mabao 634 na kutoa asisti 285 kwenye mechi 731 alizoicheza.



Sportsmail inaelewa kuwa Messi na Guardiola wamekuwa wakiwasiliana kupitia simu juu ya kutua kwake Etihad, hata kujadili jinsi Messi atakavyozoea England na kujifunza Kiingereza baada ya miaka 20 Hispania.

 

Wazo la kumsajili Messi kwa muda mrefu lilionekana kama ndoto isiyowezekana lakini dau la pauni milioni 89.5 kujumlisha Silva, Jesus na Garcia linaweza kufanya usajili huo utimie.



Comments

Popular posts from this blog

SIMBA NA YANGA MSIBEBE MATOKEO UWANJANI

FT: VPL:SIMBA 4-0 IHEFU

WAMEANZA NA MAJANGA MSIMU MPYA WA 2021/22, SIMBA WANAWEZA KUKOSA UBINGWA